DC KUBECHA AZINDUA MRADI WA E360 WA UWEZESHAJI UJASIRIAMALI WA WANANCHI WALIOGUSWA NA MRADI WA BOMBA LA MAFUTA, -


Mkuu wa wilaya ya Tanga Mhe Japhari Kubecha  Amezindua mafunzo ya Mradi wa E360 wa Uwezeshaji wa Ujasiriamali kwa Wananchi ambao Waliguswa na mradi wa Bomba la Mafuta ,

Mafunzo hayo Yalishirikisha Watu Mbalimbali Wenyeviti wa Mitaa ,Watendaji wa Kata na Mitaa ambao Mradi Huu Umepita , Pia Viongozi wa Dini Pamoja na Wananchi ambao Mradi wa Bomba la Mafuta Uliwagusa ,

Aidha Mkuu wa wilaya Amewaomba washiriki Kupokea mafunzo haya ya Uwezeshaji Kiuchumi na Ujasiriamali ili Waweze Kunufaika na Kuweza Kuwa na Tija kwani Kupitia Mradi Wa Bomba la Mafuta Wameweza kupata Fursa mbalimbali na Kujikwamua Kiuchumi ,

Pia Ametoa Rai kwa Yeyote Yule Kutokwamisha Mradii Huu wa Bomba La Mafuta kwani Ni Mradi Mkubwa sana kwa Nchi yetu na Unatija kubwa sana na Kuendelea kuwasisitiza Wenyeviti wa Mitaa Kutokuwa Kikwazo kwenye Maendeleo ya Mradi  na Yeyote Yule ambaye Atakwamisha Serikali ya Wilaya Haitokuwa Tayari Kukubaliana naye .

# TANGA YETU,LANGO LA UCHUMI WA AFRIKA MASHARIKI


Bumbuli wamshukuru January Makamba kwa kutatua kero,waahidi kumchagua tena

Wakizungumza wakati wa ziara ya Mbunge huyo ya kusikiliza kero na kutoa majawabu aliyoifanya katika kila kijiji cha jimbo hilo, wananchi wamesema jitihada anazozifanya Mbunge wao kutatua changamoto katika sekta zote, wanasisitiza kuwa lazima wamchague tena.


" Sisi wananchi wa Bumbuli hatuna deni na wewe kwa sababu umetufanyia mengi, tena mengine kwa pesa zako za mfukoni. Hivyo, sisi tunaenda na wewe na hatutokuacha. Jibu letu utalipata Oktoba kwenye sanduku la kura," alisema Christina Kupaza, mkazi wa Vuga.

Said Dhahabu, mkazi wa kijiji cha Manga Funta, alieleza sababu za kumchagua tena Mbunge huyo kutokana na namna alivyoisaidia jamii yao kutatua tatizo kubwa la maji, ambalo awali lililazimu wananchi hao kutembea umbali wa kilometa nne juu ya mlima ili kufuata maji.

" Ndoa zetu ziliyumba kwa sababu wake zetu walikuwa wanatembea usiku kuchota maji. Lakini baada ya Mbunge wetu kusikia kilio chetu, alituletea rola za maji, sasa tunapata maji ya bomba majumbani mwetu, na wengine wanachota karibu na nyumba zao," alisema Said Dhahabu.

Mariam Mdoe alieleza kuwa changamoto ya maji ilipelekea baadhi ya wasichana kukosa wachumba, kwani wanaume wa mjini walikuwa wakidai hawezi kuwaoa wakati kwao hakuna maji. Hata hivyo, sasa wanapata huduma hiyo kwa urahisi baada ya Mbunge kuwapelekea maji.

Diwani wa Kata ya Funta, Francis Kanju, alisisitiza kuwa kwa yale aliyoyafanya Mbunge huyo, bora yeye asipate udiwani, lakini wamchague tena January Makamba ili aendelee kuwaongoza kwa kipindi kingine cha miaka mitano.

Diwani wa Kata ya Vuga, Jumaa Dhahabu, alifafanua kuwa Mbunge huyo ni kiongozi wa kipekee ambaye anaweza kuwasaidia wananchi wake bila kusubiri serikali.

Aliongeza kuwa katika Kata ya Vuga, Mbunge amefanya mengi ikiwemo kuwajenga shule, zahanati, na kutatua changamoto ya umeme ambapo kila kijiji kimepata umeme, kasoro vitongoji vichache ambavyo tayari ameahidi vitapata umeme. Aidha, aliendelea kusema kwamba miradi mikubwa ya maji imeanzishwa, na wananchi wameshuhudia mabadiliko makubwa baada ya mbunge huyo kuwaongoza

" Mbunge wetu, hata kama hutatokea siku ya uchaguzi, leta shati tu, tutalichagua maana umefanya mengi ambayo hayajawahi kufanywa na Mbunge mwingine aliyepita," alieleza Diwani wa Vuga, ambaye pia ni Mwenyekiti wa kudumu wa Kamati ya Elimu, Afya, na Maji katika Halmashauri ya Bumbuli.

Wananchi wengine kutoka Mgwashi na kata ya Kongoi walieleza kuwa hawana shaka ya kumchagua tena Mbunge wao wakati wa uchaguzi mkuu ujao, kwa kuwa amewafanyia mengi katika sekta zote muhimu. Hata hivyo, walieleza kuwa wanatarajia utatuzi wa changamoto ndogo ndogo zinazohusiana na barabara.

Hassani Kupaza kutoka kata ya Tamota alisisitiza kuwa Mbunge wao anastahili kupata miaka mitano mingine ya uongozi, kwa sababu tangu dunia iumbwe, kijiji chao hakikuwa na umeme wala huduma zingine. Lakini sasa huduma hizi zinapatikana kwa urahisi, ingawa changamoto hazijaisha, wameweza kutatua asilimia kubwa ya matatizo.

Kaimu Meneja wa Wakala wa Mjai vijijini (RUWASA) wilaya ya Lushoto Seleman Mdoe amesema katika Halmashauri ya Bumbuli jumla ya miradi Miwili ya maji yenye thaman ya sh.3.9 billion inaendelea kutekelezwa nakwmaba itakapokamilika jumla ya vijiji 10 vitanufaika.




RC BATILDA AWATAKA WAKAZI WA TANGA KUJIEPUSHA NA VIASHIRIA VYA UVUNJIFU WA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI



Na Hadija Bagasha Tanga,

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt. Batilda Burian amewataka wakazi Mkoani Tanga kujiepusha na vitendo vyote vinavyoashiria uvunjifu wa amani katika kipindi hiki ambacho Taifa linaelekea katika Uchaguzi wa Serikali za mitaa na uchaguzi Mkuu baadae mwakani.

Balozi Dkt.  Batilda ametoa wito huo Septemba 22,2024 katika kilele cha tamasha kubwa la Utalii wilayani Lushoto la USAMBARA TOURISM FESTIVAL lililofanyika kwa siku mbili katika viwanja vya Nyerere Square, ambapo amesema ni jukumu la kila mwanatanga kuhakikisha amekuwa sehemu ya amani na utulivu kuanzia kipindi hiki ambacho wananchi wameanza kujiandikisha katika daftari la mpiga kura ili kupata nafasi ya kuchagua viongozi makini watakao waongoza na kuwaletea maendeleo ya kweli.

Katika hatua nyingine Balozi Dkt. Batilda amewataka waratibu na wasimamizi wa uchaguzi kuhakikisha wanaweka juhudi katika kutoa elimu na kuwashirikisha wananchi wa ngazi zote ikiwemo viongozi wa kimila na waandishi wa vyombo vya habari katika kutoa elimu ya uchaguzi.

Awali akizungumzia Utalii Dkt.Batilda amesema Wilaya ya Lushoto imebarikiwa kwa vivutio mbalimbali vya utalii na hivyo kuwa sehemu ya kichocheo cha maendeleo na kupongeza uongozi wa Wilaya ya Lushoto kufanikisha ujenzi wa kituo cha utalii ambacho kitasaidia upatikanaji wa taarifa muhimu za utalii.

Amewaelekeza viongozi wa Wilaya zingine za Mkoa wa Tanga kuwa na vituo vya utalii ili kurahisisha upatikanaji wa taarifa kwa wageni wanaotembelea maeneo hayo.

Akizungumza kwa niaba ya Benki ya NMB Meneja Mahusiano wa Benki ya NMB na Serikali Peter Massawe amesema Benki hiyo ipo katika mchakato wa kusaidia sekta ya Utalii kwa kukaa na watenda kazi wa Sekta hiyo na kuona wanauhitaji wa mambo gani na kiasi gani ili kushirikiana kwa pamoja kukuza Sekta hii.

Tamasha la Usambara Tourism Festival limefanyika kwa mara ya kwanza Wilayani Lushoto na kuhusisha shughuli mbalimbali ikiwemo kutembelea vivutio vya utalii, maonesho ya biashara, shughuli za taasisi mbalimbali na kufanyika kwa mbio Usambara Marathoni kwa washiriki wa Km 21, Km 10 na KM 5 mbio zilizo ongozwa na mkuu wa Wilaya ya Lushoto Zephania Sumaye

DC PANGANI ASISITIZA MATUMIZI YA MFUMO WA GoTHOMIS VITUO VYOTE VYA AFYA.

Mkuu wa Wilaya ya Pangani mhe Mussa Kilakala  amefanya ziara yake ya kikazi ya kukagua ujenzi wa miundombinu ya vyoo vya watumishi,ujenzi wa kinawia mikono pamoja na kichomea taka katika Zahanati ya Kipumbwi.

Hayo yamefanyika leo Julai 10,2024 ambapo amesisitiza matumizi  ya mfumo wa usimamizi wa Sekta ya Afya (GoTHOMIS).

Akizungumza mala baada ya ukaguzi wa miundombinu hiyo mhe Mussa Kilakala ameeleza kuwa kwenye matumizi ya GoTHOMIS kwenye vituo vya kutolea huduma za afya, ni takwa la Serikali na kila Zahanati ihakikishe inatumia mfumo huo.

Ikumbukwe kuwa GoTHOMIS ni mfumo wa kumeneji taarifa na kukusanyia mapato ambao licha ya kuthibiti ukusanyaji wa Mapato lakini pia unasaidia kutunza kumbukumbu za matibabu ya wagonjwa, wanaofika kituoni kupata huduma mbalimbali.


 


RC SHIGELLA MGENI RASMI TANGA CITY MARATHON JUMAMOSI WIKI HII MJINI TANGA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mratibu wa Mashindano ya Riadha ya Tanga City Marathon, Juma Mwajasho kulia akitetea jambo na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya kuelekea mashindano hayo Jumamosi wiki hiikushoto ni Meneja wa Mkwabi Super Market ya Jijini Tanga ambao niwaandaaji wakuu wa mbio hizo,Kawkab Hussein na Katibu wa Chama cha Riadha Mkoani Tanga (RT) Hassan Mwagomba
Katibu wa Chama cha Riadhaa Mkoa wa Tanga (RT) Hassan Mwagomba akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na uwepo wawashiriki kutoka Visiwa vya Shelisheli, Unguja na Pemba ambao watapat afursa ya kuonyesha umahiri wao kulia ni Meneja wa Mkwabi Super Marketya Jijini Tanga ambao ni waandaaji wakuu wa mbio hizo,Kawkab Hussein,
Meneja wa Mkwabi Super Market ya Jijini Tanga ambao ni waandaaji wakuu wa mbio hizo, KawkabHussein akizungumza na waandishi wa habari kwenye mkutano huu kuhusiana na zawadi zitakazotolewa msimu huu
Sehemu ya medali zitakazotolewa kwenye mashindano hayo



MKUU wa mkoa wa Tanga, Martine Shigella ametarajiwa kushuhudia mashindano ya riadha ya Tanga City Marathon msimu wa piliyanayotazamiwa kufanyika Jumamosi wiki hii mjini hapa.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mratibu wa Mashindano hayo, Juma Mwajasho alisema maandalizi yamekamilika kwa asilimia kubwa huku baadhi ya washiriki wakithibitisha kushiriki.

Alisema katika mashindano hayo msimu huu watazamia washiriki zaidi ya600 ambapo washindi watakabidhiwa zawadi mbalimbali zikiwemo medali ambazo zimeandaliwa na wadhamini wa mashindano hayo.

Aidha alisema mashindano hayo yatashirikisha wakimbaji kwenye umbali wa kilomita 21,10 na 5 ambapo wataanzia mbio hizo kwenye eneo la Mkwabi Super Market kuzunguka maeneo mbalimbali Jijini Tanga na kuishia eneo hilo.

“Lakini kwa mara ya kwanza washiriki wote watakaoshiriki mashindano hayo watapewa medali na mgeni rasmi kwenye mashindano hayo.Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Riadhaa Mkoa wa Tanga (RT) Hassan Mwagomba alisema mashindano hayo pia yatashirikisha washiriki kutoka Visiwa vya Shelisheli, Unguja na Pemba ambao watapata fursa yakuonyesha umahiri wao.

Alisema njia zitakazopitia mashindano hayo zimeboreshwa zaidi kiusalama kwa wakimbiaji ili kuweza kuepukana na adhari zinazoweza kujitokeza wakati yakiendelea.Naye kwa upande wake,Meneja wa Mkwabi Super Market ya Jijini Tanga ambao ni waandaaji wakuu wa mbio hizo,Kawkab Hussein alisema msimu huo wameboresha mashindano hayo kwa kutoa zawadi kwa mshindi wa kwanza hadi wa kumi.

Alizitaja zawadi zinazotolewa kuwa ni mshindi wa kwanza km 21 atapata700,000 wa pili 500,000, huku mshindi wa tatu akipata 300,000 huku wengine kuanzia wa nne hadi wa kumi watapata kifuta jasho cha 50,000.

Hata hivyo alisema katika kilomita 10 mshindi wa kwanza atapata 250,000, wa pili 150,000 na wa tatu 100,000 huku washindi wa kuanzia nafasi ya nne mpaka 10 watapewa 30,000 pia kutakuwa na vituo maalumu kwaajili ya kutoa huduma ya maji kwa wakimbiaji (Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha)

NAIBU WAZIRI AWESO SIPO TAYARI KUONA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO ZINATUMIKA VIBAYA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso kushoto akimsikiliza kwa umakini Mkandarasi kutoka Kampuni ya Wesers Limited ambaye anasimamia mradi wa ujenzi wa jengo la Halmashauri ya wilaya ya Pangani Kisyeri Chambiri mara baada ya kulitembelea kuona namna linavyoendelea wakati wa ziara yake ambapo alihimiza likamilike kwa wakati kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Pangani
 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso kushoto akimueleza jambo  Mkandarasi kutoka Kampuni ya Wesers Limited ambaye anasimamia mradi wa ujenzi wa jengo la Halmashauri ya wilaya ya Pangani Kisyeri Chambiri mara baada ya kulitembelea kuona namna linavyoendelea wakati wa ziara yake ambapo alihimiza likamilike kwa wakati.
 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso kushoto akisisitiza jambo kwa umakini Mkandarasi kutoka Kampuni ya Wesers Limited ambaye anasimamia mradi wa ujenzi wa jengo la Halmashauri ya wilaya ya Pangani Kisyeri Chambiri mara baada ya kulitembelea kuona namna linavyoendelea wakati wa ziara yake ambapo alihimiza likamilike kwa wakati
 Mkuu wa wilaya ya Pangani,Zainabu Abdallah akizungumza katika ziara hiyo kulia Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Pangani,Sabas Chambasi
 Sehemu ya jengo la Halmashauri ya wilaya ya Pangani ambalo ujenzi wake unaendelea

 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) akikagua ujenzi wa Jengo la Halmashauri ya wilaya hiyo kuweza kuona namna inavyoendelea

  Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) akikagua ujenzi wa Jengo la Halmashauri ya wilaya hiyo kuweza kuona namna inavyoendelea
 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) akikagua ujenzi wa Jengo la Halmashauri ya wilaya hiyo kuweza kuona namna inavyoendelea
  Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) akitoka kwenye eneo la ujenzi wa  Jengo la Halmashauri ya wilaya hiyo kuweza kuona namna inavyoendelea

 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) akisalimiana na mmoja wa wakina mama wanaofanya kazi kwenye ujenzi wa Jengo la Halmashauri ya wilaya hiyo kuweza kuona namna inavyoendelea

 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) akitembelea maeneo mbalimbali mara baada ya kukagua ujenzi wa jengo la Halmashauri hiyo kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Pangani,Seif Ally katikati ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Issa
 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM)akisalimiana na wakazi wa Mji huo kabla ya kuvuka kivuko kuelekea upande wa pili wilayani Pangani akiwa kwenye ziara yake

 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM)kulia akiingia kwenye kivuko cha kuvuka mto Pangani kuelelea ng'ambo ya pili ya mji wa Pangani wakati wa ziara yake

 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM)wa pili kushoto akifurahia jambo na mmoja wa wananchi wakati akiwa kwenye kivuko cha Mto Pangani kuelelea ng'ambo ya pili ya mji wa Pangani kwa ajili ya kufanya ziara kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Issa


Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) akishuka kwenye kivuko kuelekea ng'ambo ya pili ya mto Pangani kuendelea na ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo


NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso amesema hatakuwa tayari kuona fedha za miradi ya maendeleo zinatumika vibaya huku akimtaka Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Sabasi Chambasi kuwa makini nayo.

Hatua hiyo inatokana na kuwepo kwa baadhi ya miradi inayotekelezwa kwenye maeneo mbalimbali kujengwa chini ya kiwango jambo ambalo linasababishwa na kutokuwa makini kwa viongozi wanaoisimamia.

Aweso aliyasema hayo wakati alipotembelea mradi wa ujenzi wa jengo la Halmashauri ya wilaya ya Pangani ambalo limegharimu kiasi cha milioni 600 linalosimamiwa mkandarasi Kisyeri Chambiri kutoka kampuni ya Wesers Limited.

Alisema mradi huo una umuhimu mkubwa sana kwa wilaya hiyo hivyo lazima watumishi wakiwemo wale ambao wanasimamia suala hilo kuhakikisha wanatimiza wajibu wao ili kuweza kuongeza ufanisi wakati wakitekeleza suala hilo.

“Mkandarasi huu mradi ni muhimu sana kwa Halmashauri yetu hivyo sitopenda kuona unajengwa chini ya kiwango lakini pia hakikisheni unakamilika kwa wakati kwa lengo la kufanya kazi “Alisema.

Naibu Waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) alimuagiza mkurugenzi huyo kuweka umakini mkubwa kwenye ujenzi huo ili kuepukana na utekekelezaji wake kuwa chini ya kiwango kutokana na kutumia fedha nyingi.

Hata hivyo alimwambia Mkurugenzi huyo wa Pangani kuhakikisha anamsimamia vizuri mhandisi mshauri wa mradi huo ambae ni mwajiriwa wa Halmashauri hiyo ili ukamilike kwa wakati na kuondoa adha kwa watumishi ya kutokua na Halmashauri yenye ubora.

“Si kitu cha busara kuona mhandisi mshauri ambae ni mtu muhimu katika mradi huo kutokuonekana, Mkurugenzi ninamashaka na mradi huu kama kweli utakamilika kwa muda uliopamnga ambapo ni mwezi Juni mwaka huu”Alisema.

Hata hivyo aliwatahadharisha viongozi wa Halmashauru kuwa makini na matumizi ya fedha za Serikali ambazo zinatolewa na Serikali au wadau mbalimbali wa maendeleo kwani bila kufanya hivyo wanaweza kuzorotesha maendeleo (Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

CHATANDA AWAWASHIA 'MOTO' WAHANDISI WA MAJI HALMASHAURI YA MJI KOROGWE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
PICHANI: Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini mkoani Tanga (CCM) Mary Chatanda (kushoto) leo Februari 28, 2018 amefika Mtaa wa Kwanduli, Kata ya Bagamoyo katika Halmashauri ya Mji Korogwe kuangalia miradi mbalimbali ikiwemo ule wa umeme kwenye vitongoji sita vya Mtaa wa Kwanduli unaotekelezwa kupitia Wakala wa Umeme Vijijini (REA). Pichani anaangalia nguzo ambapo wakati wowote zitasimikwa. (Picha na Yusuph Mussa).

Na Yusuph Mussa, Korogwe
IMMAMATUKIO

MBUNGE wa Jimbo la Korogwe Mjini Mary Chatanda amesema kitendo cha wananchi wa Kitongoji cha Kwatomokwe, Mtaa wa Kwanduli, Kata ya Bagamoyo katika Halmashauri ya Mji Korogwe mkoani Tanga kuwekewa vilula vya kuchotea maji, wakati maji hayo hayatoki, huo ni ubadhirifu wa fedha za umma.

Alisema chanzo cha kukosekana maji hayo ni kutega mabomba kwenye vyanzo vya maji ambavyo havina uhakika, ndiyo maana mradi huo uliokamilika katikati ya Januari, mwaka huu, ulitoa maji siku ya ufunguzi, lakini baada ya hapo, maji hayajatoka tena.

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa