Home » » NAIBU WAZIRI AWESO SIPO TAYARI KUONA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO ZINATUMIKA VIBAYA

NAIBU WAZIRI AWESO SIPO TAYARI KUONA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO ZINATUMIKA VIBAYA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso kushoto akimsikiliza kwa umakini Mkandarasi kutoka Kampuni ya Wesers Limited ambaye anasimamia mradi wa ujenzi wa jengo la Halmashauri ya wilaya ya Pangani Kisyeri Chambiri mara baada ya kulitembelea kuona namna linavyoendelea wakati wa ziara yake ambapo alihimiza likamilike kwa wakati kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Pangani
 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso kushoto akimueleza jambo  Mkandarasi kutoka Kampuni ya Wesers Limited ambaye anasimamia mradi wa ujenzi wa jengo la Halmashauri ya wilaya ya Pangani Kisyeri Chambiri mara baada ya kulitembelea kuona namna linavyoendelea wakati wa ziara yake ambapo alihimiza likamilike kwa wakati.
 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso kushoto akisisitiza jambo kwa umakini Mkandarasi kutoka Kampuni ya Wesers Limited ambaye anasimamia mradi wa ujenzi wa jengo la Halmashauri ya wilaya ya Pangani Kisyeri Chambiri mara baada ya kulitembelea kuona namna linavyoendelea wakati wa ziara yake ambapo alihimiza likamilike kwa wakati
 Mkuu wa wilaya ya Pangani,Zainabu Abdallah akizungumza katika ziara hiyo kulia Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Pangani,Sabas Chambasi
 Sehemu ya jengo la Halmashauri ya wilaya ya Pangani ambalo ujenzi wake unaendelea

 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) akikagua ujenzi wa Jengo la Halmashauri ya wilaya hiyo kuweza kuona namna inavyoendelea

  Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) akikagua ujenzi wa Jengo la Halmashauri ya wilaya hiyo kuweza kuona namna inavyoendelea
 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) akikagua ujenzi wa Jengo la Halmashauri ya wilaya hiyo kuweza kuona namna inavyoendelea
  Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) akitoka kwenye eneo la ujenzi wa  Jengo la Halmashauri ya wilaya hiyo kuweza kuona namna inavyoendelea

 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) akisalimiana na mmoja wa wakina mama wanaofanya kazi kwenye ujenzi wa Jengo la Halmashauri ya wilaya hiyo kuweza kuona namna inavyoendelea

 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) akitembelea maeneo mbalimbali mara baada ya kukagua ujenzi wa jengo la Halmashauri hiyo kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Pangani,Seif Ally katikati ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Issa
 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM)akisalimiana na wakazi wa Mji huo kabla ya kuvuka kivuko kuelekea upande wa pili wilayani Pangani akiwa kwenye ziara yake

 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM)kulia akiingia kwenye kivuko cha kuvuka mto Pangani kuelelea ng'ambo ya pili ya mji wa Pangani wakati wa ziara yake

 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM)wa pili kushoto akifurahia jambo na mmoja wa wananchi wakati akiwa kwenye kivuko cha Mto Pangani kuelelea ng'ambo ya pili ya mji wa Pangani kwa ajili ya kufanya ziara kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Issa


Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) akishuka kwenye kivuko kuelekea ng'ambo ya pili ya mto Pangani kuendelea na ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo


NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso amesema hatakuwa tayari kuona fedha za miradi ya maendeleo zinatumika vibaya huku akimtaka Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Sabasi Chambasi kuwa makini nayo.

Hatua hiyo inatokana na kuwepo kwa baadhi ya miradi inayotekelezwa kwenye maeneo mbalimbali kujengwa chini ya kiwango jambo ambalo linasababishwa na kutokuwa makini kwa viongozi wanaoisimamia.

Aweso aliyasema hayo wakati alipotembelea mradi wa ujenzi wa jengo la Halmashauri ya wilaya ya Pangani ambalo limegharimu kiasi cha milioni 600 linalosimamiwa mkandarasi Kisyeri Chambiri kutoka kampuni ya Wesers Limited.

Alisema mradi huo una umuhimu mkubwa sana kwa wilaya hiyo hivyo lazima watumishi wakiwemo wale ambao wanasimamia suala hilo kuhakikisha wanatimiza wajibu wao ili kuweza kuongeza ufanisi wakati wakitekeleza suala hilo.

“Mkandarasi huu mradi ni muhimu sana kwa Halmashauri yetu hivyo sitopenda kuona unajengwa chini ya kiwango lakini pia hakikisheni unakamilika kwa wakati kwa lengo la kufanya kazi “Alisema.

Naibu Waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) alimuagiza mkurugenzi huyo kuweka umakini mkubwa kwenye ujenzi huo ili kuepukana na utekekelezaji wake kuwa chini ya kiwango kutokana na kutumia fedha nyingi.

Hata hivyo alimwambia Mkurugenzi huyo wa Pangani kuhakikisha anamsimamia vizuri mhandisi mshauri wa mradi huo ambae ni mwajiriwa wa Halmashauri hiyo ili ukamilike kwa wakati na kuondoa adha kwa watumishi ya kutokua na Halmashauri yenye ubora.

“Si kitu cha busara kuona mhandisi mshauri ambae ni mtu muhimu katika mradi huo kutokuonekana, Mkurugenzi ninamashaka na mradi huu kama kweli utakamilika kwa muda uliopamnga ambapo ni mwezi Juni mwaka huu”Alisema.

Hata hivyo aliwatahadharisha viongozi wa Halmashauru kuwa makini na matumizi ya fedha za Serikali ambazo zinatolewa na Serikali au wadau mbalimbali wa maendeleo kwani bila kufanya hivyo wanaweza kuzorotesha maendeleo (Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa