Home » » MSIPOTUMIA FURSA ZILIZOPO TANGA WAGENI WATAZITUMIA-DKT. MWAKYEMBE

MSIPOTUMIA FURSA ZILIZOPO TANGA WAGENI WATAZITUMIA-DKT. MWAKYEMBE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akiongeza wakati wa ufunguzi wa Jukwaa la Fursa za Kibiashsra lililofanyika leo Jijini Tanga. Jukwaa hilo lilijadili fursa mbalimbali za kibiashara zinazopatikana Mkoani Tanga.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martin Shigela akitoa neon la utangulizi wakati wa ufunguzi wa ufunguzi wa Jukwaa la Fursa za Kibiashsra lililofanyika leo Jijini Tanga. Jukwaa hilo lilijadili fursa mbalimbali za kibiashara zinazopatikana Mkoani Tanga
Mhariri Mtendaji wa Tanzania Standard Newspapers Dkt. Jim Yonaz akielezea kuhusu malengo ya kongamano la Jukwaa la Fursa za Kibiashsra lililofanyika leo Jijini Tanga. Jukwaa hilo lilijadili fursa mbalimbali za kibiashara zinazopatikana Mkoani Tanga.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezi, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amewataka wakazi wa na wafanyabiashara wa Mkoa wa Tanga kuanza mapema kuzitumia fursa zilizopo katika mkoa huo kabla ya wageni hawajazitu,ia na kuwaacha wenyeji kuwa watazamaji.

Waziri Mwakyembe ametoa rai hiyo leo Jijini Tanga wakati akifungua kongamano la siku moja la Fursa za Biashara ambalo lina lengo la kufungua fursa za biashara zilizopo katika mkoa na hasa katika kipindi hiki ambacho ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani jijini Tanga unatarajiwa kuanza.

“Tusipojipanga leo na kuzitumia vizuri hizi fursa nyingi zilizopo basi tujue fursa hizi zitatumiwa na wageni ili hali Watanzania tunaauwezo”, alisisitiza Waziri Mwakyembe.

Alieleza kuwa kama kuna changamoto zozote zinazowakabili watu wa Tanga na Watanzania kwa ujumla katika kutumia fursa zilizopo basi ni vema Serikali ya Mkoa, wafanyabishara na wawekezaji waliopo mkoa wa Tanga wakazitafutia ufumbuzi changamoto hizo ili zigeuke kuwa fursa ili Watanzania wazichangamikie.

Aidha Mwakyembe amewasisitiza Watanzania kuwekeza katika biashara ya huduma na viwanda vya uzalishaji bidhaana bidha ambapo vitakuwa vikihudumia ujenzi wa miradi mbalimbali hususani bomba la mafuta kutoka Hoima-Uganda hadi Chongoleani-Tanga, Tanzania

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa