Home » » MCHANGANYIKO ASALI & MDALASINI INAOTESHA NYWELE, NGUVU ZA KIUME IMARA

MCHANGANYIKO ASALI & MDALASINI INAOTESHA NYWELE, NGUVU ZA KIUME IMARA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.



SEHEMU ya kwanza ya makala hii, Alhamisi iliyopita, ilionyesha orodha ndefu ya maajabu ya tiba itokanayo na mchanganyiko wa asali na mdalasini. Ufuatao ni mwendelezo wa tiba za mchanganyiko huo uliotajwa:

Tiba ya kansa; Ingawa bado haijathibitishwa kisayansi namna asali yenye mdalasini inatibu kansa, lakini uwezo wake wa kuondoa sumu na vimelea vingine vya magonjwa (free radicals) inaipa asali sifa ya kutibu kansa.

Wapo watu wamesharipoti kupona kansa ya titi na kansa ya utumbo mpana, kwa kutumia asali yenye mdalasini.

Inaongeza nguvu ya mwili; Asali ina madini na vitamini nyingi ndani yake, wakati mdalasini wenyewe ina Kalsium (calcium), chuma, vitamini C, vitamini K, maangamizi na nyuzinyuzi (fiber).

Vinapoungana vitu hivyo viwili, inaunda dawa muhimu sana ya kuongeza kinga ya mwili. Mtu akinywa chai yenye mdalasini kila mara, kwani inaongeza kinga ya mwili, nguvu ya mwili na nguvu ya ubongo kufanya kazi.

Hutibu chunusi; Kupakaa asali yenye mdalasini kwenye ngozi yenye chunusi, inasaidia kuondoa chunusi hizo bila ya kuchelewa. Asali inawadhibiti bakteria na mdalasini hudhibiti maambukizi na huondoa sumu.

Mchanganganyiko huo unasaidia asali kubaki juu ya ngozi kwa muda mrefu na hivyo kuleta uponyaji unaohitajika.

Tiba ya kikohozi; Mtu akinywa asali yenye mdalasini ndani ya glasi ya maji ya vuguvugu, hupunguza vyote, kikohozi na kikohozi kikavu. Pia, inasafisha msongamano kooni na kutibu kikohozi cha kawaida, pia kikavu.

Inazuia madhara ya kung’atwa na wadudu; Ni nzuri kwa ajili ya uvimbe au kuondoa maumivu yatokanayo na kuumwa na wadudu. 

Namna ya kutumia ni kwamba, mtu anachukua kijiko kidogo cha asali na achanganye ndani ya vijiko viwili vya maji na kisha anaongeza mdalasini ya unga, nusu kijiko cha chai kisha anatakiwa apake juu ya sehemu alipong’atwa na mdudu. Maumivu hayo huondoka mara moja.

Inasaidia kuotesha nywele; Namna ya kutumia, inaanza kwa kuchanganya kijiko kidogo kimoja cha asali ndani ujazo sawa na mafuta ya zeituni. Kisha mtumiaji huyo aongeze kijiko kidogo cha chai tena cha mdalasini ya unga kwenye huo mchanganyiko.

Baada ya hapo, hatua inayofuata ni kupakaa mchanganyiko huo kichwani katika sehemu ambako nywele zimeanza kupotea.

Kinachofuata ni kwamba, dawa hiyo inaachwa mahali hapo kwa muda wa dakika 15 na kisha mhusika anajisafisha na maji ya vuguvugu, pia shampoo ya asili.


Inatibu lehemu (Cholesterol); Matumizi ya mara kwa mara ya asali yenye mdalasini inasaidia kupunguza lehemu. Pia, inasaidia kushusha shinikizo la juu la damu na kusafisha ateri (mishipa midogo mwilini) inayoziba.

Mchanganyiko huo unabadili matumizi ya mafuta mengine kwa kutumia mafuta ya zeituni kurahisisha kuweka sawa kolestro iliyo mwilini.

Tiba ya maumivu ya jino: Inafanyikaje? Mtu anatakiwa kuchanganya kijiko kidogo kimoja cha chai chenye mdalasini ya unga na vijiko vikubwa viwili vya asali mbichi na kisha ipake kidogo kidogo juu ya jino linalouma mara kadhaa kila siku, mpaka maumivu yatakapotoweka.

Harufu mbaya mdomoni; Tiba yake hufanyika kwa kuchanganya kijiko kikubwa kimoja cha asali na kiasi kingine kama hicho cha mdalasini ya unga ndani ya maji glasi moja ya vuguvugu na mgonjwa anywe kila anapoamka asubuhi. Hiyo ni tiba dhidi ya harufu mbaya mdomoni na anapumua vizuri, bila ya shida yoyote.

Tiba kwa kushindwa tendo la ndoa au kukosekana hamu ya kufanya hivyo; Inaelezwa, jaribu uone tofauti! Kwa vipi? Changanya vijiko vikubwa vitatu vya asali yenye mdalasini ndani ya glasi moja ya maji ya vuguvugu na uache mchanganyiko huo kwa dakika 15 hivi.

Kunywa nusu glasi kila asubuhi kabla ya mlo wa asubuhi na nusu nyingine, kabla ya kwenda kulala kwa siku kadhaa hata wiki kadhaa.

Inaongeza kinga ya mwili; Ongeza kinga yako ya mwili na magonjwa hayatakugusa. Kwa Asali na mdalasini hupigana dhidi ya bakteria na virusi na kufanya iwe dawa nzuri sana.
Asali ina madini na vitamini muhimu na nyingi, hivyo inaupa mwili viinilishe muhimu vinavyohitajika.
Tiba ya mafua: Mafua ni maradhi ya wengi. Mtu anapotumia mchanganyiko wa kijiko kimoja cha chakula cha asali yenye mdalasini ndani ya glasi moja ya maji ya vuguvugu, kwa kipimo cha kutwa mara moja kila siku, inaondoa chafya na kuvimba koo.

Hutibu ugumba; Asali inaaminika kuamsha hamu ya mapenzi. Wapenzi wa jinsia zote wanashauriwa kunywa walau vijiko viwili vya chakula kila siku, kabla ya kwenda kulala kwa siku hiyo.

Mdalasini imetumika kwa miaka mingi katika dawa za Kichina na Kihindi, kuongeza uwezo wa uzazi kwa kinamama wanaohitaji uzazi. 
Chanzo:Nipashe

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa