Home » » PROF DOS SANTOS KUWASILISHA MADA YA UHIFADHI WA MISITU NA MPANGO MKAKATI WA UTALII NCHINI

PROF DOS SANTOS KUWASILISHA MADA YA UHIFADHI WA MISITU NA MPANGO MKAKATI WA UTALII NCHINI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.


Mtendaji Mkuu Wakala wa Huduma za Misitu (TFS), Prof. Dos Santos Silayo (kulia) akimsikiliza Mkurugenzi wa Utalii na Masoko wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania, Ibrahim Mussa (kushoto) alipokuwa akimueleza mambo mbalimbali ya uhifadhi na changomoto zake inapokuja suala la kushirikisha vyombo vya habari kabla ya kufungua mkutano wa sita wa wahariri na wanahabari waandamizi unaohusu sekta ya utalii nchini ambao umeandaliwa na Hifadhi za Taifa (TANAPA) unaofanyika jijini Tanga 27 - 29, Julai 2017. Pichani kati ni Mkurugenzi Mkuu wa Shrika la Hifadhi za Taifa,(TANAPA),Allan Kijazi 
Katika mkutano huo Prof  Silayo atawasilisha mada "uhifadhi wa misitu ya hifadhi ya asili na mpango mkakati wa utalii Kesho Ijumaa ya tarehe 28 Julai 2017 saa 05:45 asubuhi na kurushwa moja kwa moja kupitia ukurasa wa facebook wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (www.facebook.com/foresttz). 
usikose kuungana naye na atajibu maswali yatakayoibuka kutokana na mada atakayoiwakilisha!

Mratibu wa Mradi wa Misitu ya Hifadhi ya Mazingira Asilia Tanzania, Gerald Kamwenda (Kushoto) akijadiliana jambo na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Prof Dos Santos Silayo mara baada ya kupokea taarifa za wajumbe wa Mkuno Mkuu wa Mwaka wa Wahariri na Wanahabari Waandamizi ulioandaliwa na Hifadhi za Taifa Tanzania kutembelea Hifadhi ya Misitu Asilia ya Amani Siku ya Jumamosi (Julai 29,2017).

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa