Home » » WASTAAFU ANGLIKANA KUPEWA PENSHENI

WASTAAFU ANGLIKANA KUPEWA PENSHENI


KANISA la Anglikana Dayosisi ya Tanga, limeanzisha mfuko wa malipo ya uzeeni (pensheni), kwa watumishi wake yatakayowasidia baada ya kustaafu.
Hayo yalisemwa na Askofu wa Kanisa hilo, Mahimbo Mndolwa alipozungumza na Tanzania Daima wakati wa hafla ya kumuaga Mchungaji wa Kigango cha Mashewa, Thomas Ngereza iliyofanyika katika Kanisa Mtakatifu Andrews Manundu wilayani Korogwe mwishoni mwa wiki.
Askofu Mndolwa alisema kuanzishwa kwa mafao hayo kutamsaidia mhusika wakati atakapostaafu ili aepukane na maisha magumu yatakayowafanya wageuke ombaomba.
“Leo tukiongozwa na Mwenyekiti wetu Dominic Singano tumemzawadia mstaafu mabati 59; mbao, misumali kilo 10 na kumkabidhi cheti,” alisema Mndolwa.
Alitaja baadhi ya mafao atakayopatiwa mstaafu kuwa ni nyumba, gari na fedha ambayo anaamini yatamsaidia mstaafu huyo katika kupambana na changamoto za maisha.
Licha ya kumuaga mchungaji Ngereza pia walikuwepo watumishi wengine wanne waliostaafu kutoka Taasisi ya Afya na Sayansi Shirikishi ya Mtakatifu Agustino wilayani Muheza ambao ni Mery Dismasi, Charles Juma, Peter Rajabu na Itikija Mbaga.
 Chanzo;Tanzania Daima
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa