Home » » MBARONI KWA WIZI WA KUTUMIA SILAHA

MBARONI KWA WIZI WA KUTUMIA SILAHA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

JESHI la Polisi Mkoa wa Tanga linawashikilia watu nane kwa tuhuma za unyang’anyi wa sh 978,600 kwa kutumia silaha katika Kijiji cha Jasini mpakani mwa Kenya na Tanzania.
Akithibitisha kutokea kwa uhalifu huo, Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Costantine Massawe, alisema ulitokea usiku wa kuamkia Juni 9, mwaka huu.
Kamanda Massawe alisema watuhumiwa hao walimvamia mfanyabiashara, Mohamed Tembo mkazi wa Jasini wakiwa na mapanga kisha kumpora pesa hizo huku akibainisha watuhumiwa sita walikamatwa na wengine wawili walitoroka.
Wakati huo huo, Jeshi la Polisi mkoani hapa linawashikilia wakazi wawili wa maeneo tofauti kwa tuhuma za kupatikana na silaha kinyume na
sheria.
Aliwataja wanaoshikiliwa kuwa ni Jeofrey Daniel (20), mkazi wa Kwanjeka na Mussa Hamis (44), mkazi wa Mtambuwe.
Kwa mujibu wa kamanda huyo, watuhumiwa hao walikutwa na silaha aina ya Rifle yenye namba 2703520; risasi mbili, ganda la risasi, panga, kisu, na bisibisi mbili na kueleza kuwa silaha hiyo ilikutwa maungoni mwa Mussa Hamisi.
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa