Home » » TCRA YATEMBELEA VITUO VYA HABARI TANGA

TCRA YATEMBELEA VITUO VYA HABARI TANGA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa kushirikiana na Kamati ya Maudhui, imefanya ziara mkoani hapa ya kutembelea vituo vya habari kwa lengo la kuangalia namna wanavyofanya shughuli zao.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Magreth Munyagi, alisema lengo la kutembelea vituo hivyo ni kujua kanuni wanazotumia katika uendeshaji wa matangazo yao.
Munyagi alisema majukumu makubwa ya kamati hiyo ni kuhakikisha wamiliki wa vituo hivyo wanasimamia kanuni na taratibu za uendeshaji wa vituo vyao kwa maslahi ya jamii na taifa kwa ujumla na si vinginevyo.
“Tumeona ni vema tukafanya ziara hii ili tuzidi kuwaelimisha na kuwakumbusha kanuni na taratibu tukiamini wengine mnakiuka kwa kutokujua,” alisema Munyagi.
Naibu Mkurugenzi Idara ya Utangazaji wa TCRA, Fredrick Ntobi, alisema wamiliki wa vyombo hivyo wanatakiwa kuhakikisha wanaboresha mazingira ya wafanyakazi wao ikiwa ni pamoja na kusimamia ipasavyo mikataba yao.
“Wamiliki wa vituo wahakikishe wafanyakazi wanaowaajiri wanakuwa na ‘professional’ na weledi katika fani waliyoisomea, ili tasnia hii izidi kukua siku hadi siku,” alisema Ntobi.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa