Home » » TAWI LA COASTAL DUNIA HOTELLAFINGULIWA

TAWI LA COASTAL DUNIA HOTELLAFINGULIWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

UONGOZI wa timu ya Coastal Union ya Tanga jana umefungua tawi la wapenzi wa klabu hiyo liitwalo Dunia Hotel lililopo Kata ya Makorora jijini hapa ikiwa ni harakati za kuimarisha umoja na mshikamano miongoni mwa wapenzi na mashabiki wa timu hiyo.
Akizungumza jijini hapa jana, Ofisa Habari wa timu hiyo, Oscar Assenga, alisema, ufunguzi wa tawi hilo ni moja kati ya mikakati ya timu hiyo kuhakikisha wanakuwa na wapenzi Mkoa mzima.
Assenga alisema, licha ya kufungua tawi hilo, bado wanaendelea na harakati za usajili wa nguvu kwenye kikosi chao, lengo likiwa ni kuwa na timu nzuri ambayo itatimiza ndoto zao za kushiriki mashindano ya makubwa yakiwemo ya Kombe la Shirikisho (CAF), siku zijazo.
Alisema, bado wanaendelea kucheza mechi mbalimbali za kirafiki, ili kuimarisha kikosi chao cha U-20, ambacho kitashiriki mashindano mbalimbali yakiwemo ya Kombe la Uhai na Rolling Stone.
Katika hatua nyingine, Assenga alisema, kikosi cha timu ya pili kinatarajiwa kufanya ziara ya kimichezo kwenye Wilaya mbalimbali, lengo likiwa kuwapa burudani wakazi wa Mkoa huu.
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa