Home » » MABAKI MKONGE KUZALISHA SUKARI

MABAKI MKONGE KUZALISHA SUKARI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
KAMPUNI ya Katani ipo kwenye hatua za mwisho za mazungumzo kuhusu ukubwa wa kiwanda cha kuzalisha sukari kutokana  na mabaki ya mkonge, itakayotumika kwa wagonjwa wenye kisukari.
Hayo yamesemwa na Mkurungezi wa Maendeleo Katani Juma Shamte alipozungumza kwenye semina ya wazi iliyofanyika kwenye viwanja vya Tangamano jinsi wakulima watavyonufaika na mkonge.
Alisema kuwa kwasasa wapo kwenye mazungumzo ya mwisho na kampuni itakayojenga kiwanda hicho nchini kwa ajili ya kuanza uzalishaji wa bidhaa hiyo hapa nchini.
Shamte alisema kiwanda hicho kitakapo kamilika ujenzi wake na kuanza kazi kitawezesha kupungua uhaba wa sukari nchini na nyingine kuuzwa kwenye masoko ya kimataifa.
Kwa upande wa mahitaji kwenye soko la dunia, Shamte alisema uhitaji wa bidhaa za mkonge umezidi kuongezeka kwa zaidi ya asilimia 15 ya bei ukilinganisha na mwaka 2000 ambapo bei ilikuwa chini.
Hata hivyo aliwahimiza wakulima kulima mkonge kwa wingi ili kujiongeza kipato maradufu kutoka na zao hilo kuwa na soko la uhakika ndani ya nchi na hata nje ya nchi.
"Mfumo wa masoko si wa kugawana mapato kwani zao hili linamuwezasha mkulima kupata mapato yake mwenyewe na kampuni ya katani kazi yake ni kumuwezesha mkulima kupata pembejeo pamoja na kumtafutia soko la uhakika la kuuza bidhaa zake,"alisema Shamte.
 Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa