Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
WANAKIJIJI wa Gare, Kata ya Magoroto wilayani Muheza, Tanga,
wameiomba serikali kuwapelekea katapila ili wamalizie ujenzi wa barabara
kuu itokayo Amani kuelekea Muheza.
Akizungumza kwa njia ya simu na Tanzania Daima Jumatano jana, katibu
wa wananchi wapenda maendeleo wa kata hiyo, Andrew Kibuyu, alisema
barabara hiyo inatoka Kijiji cha Kwamatinda kuelekea Gare
haijakarabatiwa tangu enzi ya ukoloni.
Kibuyu alisema kukamilika kwa ujenzi wa barabara hiyo
inayowaunganisha na barabara kuu ya Amani-Muheza kutasaidia kumaliza
matatizo ya wananchi hao katika shughuli za kijamii ikiwemo kufika
hospitali ya wilaya.
“Hivi sasa wakazi wa Gare tunalazimika kuwabeba wagonjwa kwenye
machela umbali wa kilometa saba hadi barabara kuu inayotoka Amani
kuelekea hospitali Teule… shida zaidi wanapata wajawazito wanapotaka
kujifungua.
“Sisi wanakijiji cha Gare tumefanya jitihada ya kujitolea nguvu zetu
kwa ajili ya kukarabati barabara hii na tayari tumefikia kilomita 3.5.
“Tumetuma nakala za barua za kuomba msaada kwa Waziri Hawa Ghasia
(Tamisemi), Mkuu wa Mkoa Tanga, Chiku Galawa, Ofisi ya Waziri Mkuu
Mizengo Pinda, Mbunge wa Muheza Herbert Mntangi na Halmashauri ya
Muheza, lengo letu ni kupatiwa katapila hilo,” alisema.
Chanzo:Mwananchi
0 comments:
Post a Comment