Home » » ASSENGA MSEMAJI MPYA COASTALI UNION

ASSENGA MSEMAJI MPYA COASTALI UNION

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
MWANDISHI wa habari wa Kampuni ya New Habari Cooperation Mkoa wa Tanga, Oscar Assenga, ameteuliwa kuwa msemaji mpya wa klabu ya Coastal Union ‘Wagosi wa Kaya’ yenye makazi yake barabara ya 11 jijini hapa.
Uteuzi huo umefanywa katika kikao cha Kamati ya Utendaji kilichoketi juzi na kupendekeza mwandishi huyo kuwa msemaji, ambaye atakuwa na jukumu la kuhakikisha klabu hiyo inatangazwa ipasavyo kwa mujibu wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa).
Awali nafasi hiyo ilikuwa ikishikiliwa na Hafidh Kido, ambaye alibwaga manyanga hivi karibuni.
Akizungumza jijini hapa jana, Katibu wa Coastal Union, Kassim El Siagi, alisema waliamua kumteua mwandishi huyo kutokana na uwajibikaji wake na kuwa mstari wa mbele kuandika habari zinazochochea maendeleo ya michezo kwa Mkoa wa Tanga kwa ujumla.
El Siagi alisema pia waliamua kufanya hivyo, kwa sababu ni mkazi wa jijini Tanga ambaye anaweza kutumia nafasi yake vizuri kwa ajili ya kutoa taarifa mbalimbali za timu hiyo kwenye vyombo husika na kwa wakati.
Katika hatua nyingine, El Siagi alisema klabu hiyo inaendelea na mchakato wa kuhakikisha inasajili wachezaji mahiri, ambao wataweza kuhimili mikikimikiki ya Ligi Kuu Soka Tanzania Bara msimu ujao.
 Chanzo;Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa