Home » » Wanafunzi Amboni marufuku nyumba za starehe

Wanafunzi Amboni marufuku nyumba za starehe

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
MWENYEKITI wa Kamati ya Shule ya Msingi Amboni iliyopo nje kidogo ya Jiji la Tanga, Amiri Mlugu, amepiga marufuku wanafunzi wa shule hiyo kwenda katika majumba ya starehe ikiwemo vibanda vya kuonyeshea video vilivyopo mitaani.
Mwenyekiti huyo ameeleza hayo katika kikao cha wazazi, wanafunzi na walimu  kilichofanyika shuleni hapo jana kwa ajili ya kupanga mikakati ya kuleta ufaulu mzuri kwa wanafunzi wa darasa la saba kwenye mitihani yao ijayo.
Malugu pia aliwataka wazazi na walimu kushiriki katika utekelezaji wa agizo hilo ambalo litasaidia kuwakabili wanafunzi wenye tabia kama hizo.
 Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa