Home » » Shirika kujenga zahanati Kitumbi

Shirika kujenga zahanati Kitumbi

SHIRIKA la Atomtek Nuclear Energy Track limeahidi kujenga zahanati katika Kijiji cha Kitumbi, Kata ya Mkata, Handeni, Tanga.
Kwa sababu hiyo ujenzi wa zahanati hiyo utawanufaisha wakazi wa Mkata na viunga vyake ambao katika kipindi cha miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika haijawahi kupata zahanati na kusababisha wajawazito kupoteza maisha wakati wa kujifungua.
Akizungumza na Tanzania Daima Jumatano, Mwenyekiti wa kijiji hicho, Athuman Abdallah, alilishukuru shirika hilo kwa kukubali kuwajengea zahanati hiyo huku akisema itapunguza vifo vya wajawazito na watoto.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa