Home » » Wagoma kuhama kupisha barabara

Wagoma kuhama kupisha barabara

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WAKAZI wa kaya 30 wa mitaa ya Majanimapana na Nguvumali zinazotarajiwa kubomolewa makazi yao kupisha ujenzi wa barabara zimetangaza mgogoro na serikali kwa kugoma kuhama na kumtaka Rais Jakaya Kikwete kuingilia kati.
Kwa mujibu wa kamati ya wahanga hao wameiomba serikali kupitisha barabara hiyo maarufu ‘barabara ya Museveni’ inayotokea Kenya, Tanzania na Uganda maeneo ya Mabanda ya Papa ilikokuwa imepangiwa awali au sehemu za Idara ya Ndorobo ambako hakuna makazi ya watu.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Salimu Mbughuni, alisema wakazi hao wanaitaka serikali kubadilisha muelekeo wa mradi huo na kwamba wao hawapo tayari kuhama wala kupokea fidia.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa