Home » » SARUMAGAO WAJIANDAA KUANDAMANA

SARUMAGAO WAJIANDAA KUANDAMANA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mgogoro wa wakazi wa Sarumagaoni Halmashauri ya Jiji la Tanga, wanaodai kutokana na kuhamishwa katika eneo hilo umeingia katika sura mpya baada wakazi hao kutishia kuandamana hadi ofisi za mkuu wa mkoa.
Eneo la Sarumagaoni limekuwa katika mgogoro wa muda mrefu pamoja na juhudi kutoka viongozi wa Serikali kujaribu kuutatua.
Mgogoro huo ulipamba moto baada ya kuwepo na taarifa za kuanza ujenzi wa barabara na reli kwenda Bandari Mpya ya Mwambani. Wakizungumza katika mkutano wa wananchi jana, wakazi hao walisema kwamba wamechoshwa na ukimwa wa Serikali hivyo dhamira iliyo mbele yao kwa sasa ni kufanya maandamano kwenda kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa.
Weshangazwa na ukimwa wa serikali, kwani mpaka sasa hakuna tathmini yoyote iliyofanywa jambo ambalo wananchi wanaona kama vile ni maandalizi ya kunyimwa haki yao.
“Tumeshasema na leo tunafanya hivyo tena, hatuondoki mpaka haki zetu tuzipate. Hatutaki tathmini ya kutumia darubini,” walisema zaidi.
“Baada ya kumalizika mkutano huu, tutaunda kamati ya maandalizi ya maandamano ya amani mpaka kwa Gallawa, tuna imani polisi wataturuhusu.”
 Cahnzo:Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa