WAKAZI wa Kata za Mashewa na Mkomazi, wilayani Korogwe, mkoani
Tanga wamelazimika kula mizizi ya miti na matunda ili kunusuru maisha
yao
kutokana na kukabiliwa na baa la njaa.
kutokana na kukabiliwa na baa la njaa.
Kufuatia hali hiyo, wananchi hao wameiomba serikali kupeleka chakula
cha msaada haraka kwa vijiji hivyo vilivyoathiriwa na tatizo hilo ili
kuokoa maisha yao.
cha msaada haraka kwa vijiji hivyo vilivyoathiriwa na tatizo hilo ili
kuokoa maisha yao.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Mtonibombo, Kata ya Mashewa, Nuru Tina,
alithibitisha kutokea kwa hali hiyo ambapo wananchi wamekuwa
wakishindwa kushiriki kwenye shughuli za maendeleo kutoka na ukosefu
wa chakula.
alithibitisha kutokea kwa hali hiyo ambapo wananchi wamekuwa
wakishindwa kushiriki kwenye shughuli za maendeleo kutoka na ukosefu
wa chakula.
“Ukosefu wa mvua za uhakika umesababisha kukosekana kwa chakula kwani
mahindi yaliyopandwa yote yamekauka kutokana na ukame uliosababishwa
na mvua kushindwa kunyesha kwa wakati na kuwa chache,” alisema
Tina.
Tina.
Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Kulasi, Kata ya Mashewa, Teresia Ngonyani,
alisema msaada wa haraka unahitajika kunusuru maisha ya wakazi hao.
alisema msaada wa haraka unahitajika kunusuru maisha ya wakazi hao.
Aidha, Mkuu wa Wilaya hiyo, Mrisho Gambo, alikiri kuwepo kwa tatizo
hilo na kuwa halmashauri wa wilaya hiyo inafanya tathmini ya vijiji
vilivyoathirika kwa ajili ya kupatiwa msaada.
Tayari wilaya hiyo imegawiwa zaidi ya tani 35 za chakula kiasi ambacho
ofisa kilimo na chakula wa halmashauri hiyo alikaririwa na gazeti hili akisema kuwa msaada huo hauwezi kukidhi mahitaji ya wakazi hao.
Chanzo;Mwananchi
ofisa kilimo na chakula wa halmashauri hiyo alikaririwa na gazeti hili akisema kuwa msaada huo hauwezi kukidhi mahitaji ya wakazi hao.
0 comments:
Post a Comment