Home » » VICOBA 170 VYAANZISHWA LUSHOTO

VICOBA 170 VYAANZISHWA LUSHOTO

JUMLA ya vikundi vya Vicoba 170 vyenye thamani ya zaidi ya sh milioni 600 vimeanzishwa wilayani hapa kuanzia  mwaka 2005 hadi 2009.
Mratibu wa Vicoba Wilaya ya Lushoto, Hande Mwanjela, alieleza hayo alipokuwa akitoa taarifa ya maendeleo ya Vicoba wilayani hapa na kusema kuwa walianza na vikundi 16 mwaka 2005.
Alisema wakati wote wa uhamasishaji wa uanzishwaji wa vikundi hivyo,  wanachama ndio waliopewa jukumu la kuwalipa wawezeshaji, na kwamba ushirikiano huo na wataalamu umesababisha maendeleo makubwa kwenye vikundi hivyo.
Mkufunzi wa Vicoba, Ayub Russia, alisema kuwa kikundi cha Mwongozo  ambacho wanachama wake wanapata vyeti, ni miongoni mwa vikundi 25 vilivyomo katika Tarafa ya Mlalo ambavyo vina wanachama 754.
Alisema miongoni mwa changamoto za vikundi hivyo mbali na tatizo la mitaji, ni itikadi za kidini na wanasiasa ambao wamekuwa wakitoa tafsiri zisizo sahihi kuhusu maana na dhana halisi ya Vicoba.
 Chanzo;Tanzania Daima
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa