Kilindi. Nyumba 62 zilizopo katika Vijiji vya Wilaya ya Kilindi,
zimeezuliwa na nyingine kubomoka kutokana na mvua kubwa iliyoambatana
na upepo mkali kunyesha kwenye maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Tanga.
Maafa hayo yamesababisha mtoto mmoja kufa kwa kuangukiwa na nyumba, huku zaidi ya wanavijiji 110 kukosa mahala pa kuishi.
Kwa mujibu wa habari zilizopatikana na
kuthibitishwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Selemani Liwowa ni kuwa
nyumba hizo zimeezuliwa usiku wa kuamkia Ijumaa wiki iliyopita baada ya
kunyesha mvua iliyoambatana na upepo.
Gazeti hili lilijulishwa kuwa mvua kubwa ilinyesha katika vijiji mbalimbali vya wilayani hapa na kusababisha madhara hayo.
Akithibitisha tukio hilo, Liwowa alivitaja vijiji
vilivyokumbwa na maafa hayo kuwa ni Songe, ambako mtoto mmoja amekufa
kwa kuangukiwa na ukuta.
Vijiji vingine ni Kwasetemba, ambako nyumba 16 zimeanguka na Gitu zilikobomoka na kuezuliwa ni nyumba 42.
Alisema ya maafa hayo, Kamati ya Ulinzi na Usalama
ya Wilaya Kilindi iliweza kutembelea kwa lengo la kujionea athari,
ambapo hatua inayofuata ni kutuma wataalamu kutathimini athari na
mahitaji kwa waathirika.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment