TIMU ya Mgambo JKT imejipanga kuhakikisha
haishuki daraja msimu huu na inafanya kila jitihada kufikia lengo lake hilo.
Akizungumza baada ya mchezo baina ya Timu
yake na wenyeji Rhino rangers kocha wa Mgambo JKT, Bakari Shime, amesema
wamejipanga msimu huu wasiteremke daraja huku akiwapongeza wachezaji wake kwa
kujituma na kufuata maelekezo yake.
Naye Kocha wa Rhino Rangers, Jumanne Chale, mbali
ya kuitupia lawama safu yake ya ulinzi, amesema bado hawajakata tamaa na
wanapambana kuhakikisha wanafanya vizuri msimu huu
Kwenye mchezo uliochezwa jana katika uwanja
wa Ali Haasan Mwinyi Mjini Tabora, Timu hizo zilitoka sare ya kufungana bao
moja moja
Mchezo huo ni wa tatu mfululizo kwa Timu ya
Rhino rangers kwenye uwanja wa nyumbani wa Ali Hassan Mwinyi na kuambulia
pointi mbili tu baada ya kutoka sare michezo miwili na mmoja kupoteza
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment