Home » » “Sheria kulinda siri za wateja inawalinda mapapa’

“Sheria kulinda siri za wateja inawalinda mapapa’

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
KAMANDA wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru) Mkoa wa Tanga, Edson Makallo, amesema sheria ya kulinda siri za mteja inayotumika katika taasisi za fedha ni kikwazo kwa vyombo vya upelelezi vinavyochunguza makosa ya mapapa  wanaotorosha fedha nje ya nchi.
Makallo alitoa kauli hiyo mjini hapa juzi wakati akifungua mafunzo ya wiki moja ya wakaguzi wa ndani wa Hesabu za Serikali inayofanyika Hoteli ya Mkonge.
Alisema vyombo vya upelelezi vinakumbana na vikwazo vya sheria inayotumiwa na taasisi za fedha ya kulinda siri ya mteja na kwamba mapapa wanaotorosha fedha nje ya nchi wamekuwa wakikwepa kuchunguzwa kupitia sheria hiyo.
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa