Home » » Wafugaji wamlalamikia diwani

Wafugaji wamlalamikia diwani

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WAFUGAJI  wa  Kata  ya  Kwamatuku, Wilaya ya Handeni, mkoani Tanga, wamemlalamikia diwani  wa  kata  hiyo, Mustaph  Beleko,  kuwa  anatumia vibaya agizo la Mkuu wa Wilaya hiyo, Muhingo  Rweyemamu  la kupunguza  mifugo kwa  kuendesha  zoezi hilo kwa upendeleo.
Wakizungumza na waandishi wa habari jana, wafugaji hao walisema diwani huyo ameegemea upande wa wakulima kwa lengo la kujijenga kisiasa kwenye uchaguzi mkuu ujao.
Nosa Irurai, alieleza hali hiyo  inaashiria mgogoro mkubwa  na kwamba  wafugaji  hao  wanadai kuchoshwa na  matukio ya  kikatili kwao na  mifugo yao kwa madai kuwa wanalipishwa faini ya kati ya sh 150,000 hadi 300,000 bila vikao vya kisheria.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa