Home » » Mvua yaangusha nguzo 35 za umeme

Mvua yaangusha nguzo 35 za umeme

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
MVUA iliyonyesha kwa siku mbili mfululizo ikiambatana na kimbunga, imeangusha nguzo 35 za Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na kusababisha ukosefu wa umeme kwa wilaya za Handeni na Kilindi, mkoani Tanga.
Mvua hiyo kubwa ambayo haijapata kutokea kwa miaka 10, imesababisha mafuriko kwenye vijiji vya Kwamsala, Sindeni na Misima, Handeni na kuacha hofu ya kurudi tena kwa kimbunga hicho.
Akizungumza na waandishi wa habari waliokuwa kwenye Kijiji cha Misima juzi, Meneja wa TANESCO Handeni, Emmanuel Mossy, alisema kimbunga hicho kimeisababishia hasara kwa shirika na wateja wake na kwamba haijulikani huduma ya umeme itarejea lini.
Alisema jitihada ambazo shirika hilo linazifanya ni kurejesha haraka huduma ya umeme kwa kuweka nguzo mpya baada ya awali kung’olewa na baadhi kukatika, hivyo kuwataka wateja wake kuwa wavumilivu wakati shirika hilo likijitahidi kuirejesha huduma hiyo.
 Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa