Home » » Watano wadaiwa kumiliki bunduki

Watano wadaiwa kumiliki bunduki

Korogwe ; Watu watano wanaodhaniwa kuwa majambazi wamekamatwa na polisi wilayani Korogwe mkoani Tanga kwa tuhuma za kukutwa na bunduki aina ya Shortgun na sare za polisi wakati wakijiandaa kwenda kufanya uhalifu .
Akithibitisha tukio hilo, Kamanda wa Polisi mkoani Tanga, Costantine Massawe alisema majambazi hao wamekamatwa Kijiji cha Gomba Kata ya Makuyuni wilayani hapa Desemba 28 mwaka huu saa 4:00 usiku baada ya kupata taarifa kutoka kwa msamaria mwema .
Kamanda Massawe alisema bunduki hiyo iliyokuwa na risasi tatu, ina namba ya Model-1400 MK II ambayo Taratibu Hemed ndiye anayeimiliki kihalali, lakini amekuwa akiikodisha kwa majambazi na kuletewa fedha anazotumia kulipia kibali cha silaha hiyo.
Massawe aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Zacharia Jeras {50] Mkazi wa Makanya Same Kilimanjaro , Mosses Jonasi {44} na Selemani Jaha {21} wote wakiwa wakazi wa Makanya Same mkoani Kilimanjaro ambapo walikiri kwenda kufanya uhalifu katika kijiji hicho cha Gomba.
Alitaja watuhumiwa wengine kuwa ni Taratibu Hemedi{74} ambaye ni mmiliki wa silaha hizo na sare pamoja na Hemedi Taratibu {32} ambaye ni mtoto wa mtuhumiwa anayemiliki silaha hizo na sare hizo ambazo ni za polisi.
Kamanda huyo alisema polisi inaendelea na uchunguzi ili watuhumiwa waweze kufikishwa mahakamani kujibu mashtaka yanayowakabili.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa