Home » » Polisi: Uhalifu umepungua Tanga

Polisi: Uhalifu umepungua Tanga

MAKOSA dhidi ya uhalifu wa kibinadamu katika Jiji la Tanga yamepungua kwa asilimia 2.64 kwani kwa mwaka 2012 yaliripotiwa matukio 492 ukilinganisha na mwaka 2013 ambapo yalikuwa 479.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi wa jiji hilo, Costantine Massawe alitoa taarifa ya hali ya uhalifu kwa kipindi cha kuanzia Januari hadi Novemba 2013.
Kamanda Massawe aliyataja makosa hayo kwa mwaka huu ni mauaji 85, kubaka 337, kutupa watoto 5, kulawiti 49 pamoja na wizi wa watoto 3 hali ambayo kwa mwaka 2012 ilikuwa tofauti.
Aliongeza kuwa mengine yalikuwa dhidi ya maadili ya jamii ambapo jumla ya makosa 529 kwa mwaka 2013 yaliripotiwa ukilinganisha na 557 mwaka 2012.
“Katika kipindi cha mwaka huu ulioisha kulikuwa na ongezeko la makosa ya kukutwa na bangi 196 yaliyoripotiwa ukilinganisha na mwaka 2012 ambapo yalikuwa 191, huku kosa la dawa za kulevya aina ya cocaine lilikuwa moja,” alisema.
Alisema kuwa matukio ya ajali za barabarani yameongezeka ambapo kwa mwaka uliopita matukio 28,334 ya ajali yaliripotiwa ukilinganisha na mwaka 2012 ambapo yalikuwa 26,529.
“Makosa hayo yalisababisha vifo 105 ambapo wavulana walikuwa 83 na wasichana 22, huku waliojeruhiwa kutokana na ajali hizo wakifikia 126,” alisema.
Katika hatua nyingine, jeshi hilo linawasaka watu 17 kwa kudaiwa kuhusika na tukio la vurugu wilayani Kilindi pamoja na kuhusika na vifaa vya milipuko katika Wilaya ya Handeni.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa