Muheza. Askofu mstaafu wa Anglikana Dayosisi ya Tanga, Phillip
Baji ameongoza jopo la mapadri wa kanisa hilo mkoani Tanga katika maziko
ya mama mzazi wa Mkurugenzi wa Kampuni ya MwananchiCommunications Ltd,
Tido Mhando, Jessie Nemganga Mhando (85) aliyezikwa katika makaburi ya
Kanisa la Kristo Mfalme.
Baji aliongoza ibada hiyo juzi na kuhudhuriwa na
idadi kubwa ya waumini wa kanisa hilo, lililopo katika Kitongoji cha
Mdaba Mjini Muheza na baadaye kwenye makaburi yaliyopo kwenye uwanja wa
kanisa hilo.
Mapadri walioshiriki kuendesha ibada hiyo chini ya
Baji, ni Cosmas Mhina, James Dominic, Christopher Kiango na Mchungaji
Daniel Mhando ambaye ni baba mzazi wa Tido Mhando.
Mazishi hayo yalihudhuriwa pia na viongozi mbalimbali wa Serikali, akiwamo Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu.
Akizungumza wakati wa ibada hiyo, Baji aliwataka
waumini wa dini hiyo kuiga mfano wa Jessie ambaye aliishi Kikristo
katika maisha yake yote, akiwa kiongozi wa wanawake pamoja na jamii
iliyomzunguka kwa jumla.
Katika salamu alizotoa mara baada ya mazishi,
Mhando aliwashukuru waliojitokeza kuifariji familia hiyo na hasa Kampuni
ya Mwananchi Communications Ltd ambayo ilibeba jukumu la kuushughulikia
mwili wa marehemu tangu alipofariki Jumanne iliyopita.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment