Home » » Ajali ya gari yaua sita, 21 wajeruhiwa

Ajali ya gari yaua sita, 21 wajeruhiwa

Tanga. Abiria sita wamekufa papo hapo na wengine 21 kujeruhiwa baada yabasi dogo walilokuwa wakisafiria  maarufu kama daladala kugongana usokwa uso na lori aina ya Volvo katika  eneo la Kange kwenye Barabara Kuu ya Tanga kwenda Segera.
Kwa mujibu wa habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Kamanda waPolisi  Mkoa wa Tanga,Costantine Massawe ni kuwa ajali hiyo ilitokeausiku wa kuamkia jana Jumapili saa 2.30 usiku  ambapo Hiace hiyoilikuwa ikitokea Tanga mjini kuelekea kitongoni cha Kange kilichokonje ya mji. Ajali hiyo ambayo imewashtua wakazi wa Jiji la Tanga ilihusisha Hiaceiliyokuwa ikiendeshwa na Gadiel Wilkael (44) ambaye pia ndiye mmlikialiyekufa papo hapo na Volvo yenye tela iliyokuwa imeegeshwabarabarani.
Waliokufa katika ajali hiyo kwa mujibu wa Massawe ni pamoja na derevawa Hiace ambaye pia ni mmiliki wa daladala hiyo Gabriel Wilkaeli (44) Raymond Mapunda (28), Halima Shaka(28), Mary Chilongoi (37) GloriaKidenya (1), Femida John (38) ambapo  miili hiyo imeshatambuliwa na ndugu zao.
Alisema majeruhi katika ajali hiyo walikimbizwa katika Hospitali yaMkoa wa Tanga ya Bombo kwa ajili ya matibabu.
Muuguzi wa zamu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga ya Bombo,Alice Mnkande aliifahamisha Mwananchi kuwa usiku huo walipokea miiliya marehemu sita na majeruhi 21 waliotokana na ajali hiyo ya Hiace.
Kamanda Massawe alisema chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa  Hiace hiyokutaka kupita gari nyingine ambapo alikutana na gari nyingine mbelena ndipo aliporudi ili kukwepa na akakutana Lori hilo lililokuwa mbeleyake.
“Dereva wa Hiace alitaka “ku-overtake” gari nyingine ndipo alipokutanana gari mbele yake, sasa ili arudi kwenye mstari akashindwa na matokeo yake akagongana uso kwa uso na hili lori ”, alisema.Alisema kati ya majeruhi hao 21 waliotibiwa na kurudi nyumbani  ni sita wanawake wawili na wanaume wanne na kwamba 15 bado wapo wodini wakiendelea na matibabu.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa