Home »
» WATUMISHI 7 WAFUKUZWA NA MADIWANI
WATUMISHI 7 WAFUKUZWA NA MADIWANI
Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya
ya Kilindi, mkoani Tanga, limewafukuza kazi watumishi saba akiwemo
daktari, matabibu, Maofisa Watendaji Kata na Vijiji.
Ofisa Maendeleo
ya Jamii wilayani humo, Athanas Michael alipewa karipio kali baada ya
kushindwa kuwajibika pamoja na Ofisa Kilimo Kata ya Mkindi, Ahimidiwe
Mmari.
Azimio la kuwafukuza kazi watendaji hao lilipitishwa katika
kikao cha madiwani hao ambapo Diwani wa Kata ya Tunguli, Bw. Michael
Bomphe, alisema jukumu lao ni kusimamia shughuli zote za maendeleo
pamoja na nidhamu kwa watumishi.
Bw. Bomphe ambaye ni mjumbe wa Kamati ya Nidhamu katika baraza hilo, aliwataja waliosimamishwa kazi kuwa ni
Mganga
Kituo cha Afya Songe, Dkt. Amir Juya ambaye hakuwepo kazini bila
taarifa na tabibu Rashid Mnkande ambaye hakuwepo kwenye kituo cha kazi
Zahanati ya Saunyi, siku tano.
"Wengine ni tabibu Msaidizi Kituo cha
Afya Songe, Joseph Dioniz ambaye hakuwepo kazini kuanzia Januari mosi
mwaka huu hadi Aprili na Ofisa Mtendaji Kata ya Negero, Confesi Mahimbo
aliyeshindwa kusimamia shughuli za maendeleo na kuwaachia Maofisa
Watendaji wa vijiji kuuza ardhi kiholela.
Aliwataja wengine kuwa ni
Mtendaji wa Kijiji cha Lwande, Abdom Jaffu kwa utoro kuanzia Juni 6,
2012 hadi Julai mwaka huu, Cuthbert Kaale ambaye ni Mtendaji wa Kijiji
cha Negero, ambaye hakuwepo eneo la kazi siku tano na Ofisa Mtendaji
Kijiji cha Mafulila, Piason Mhini aliyeshindwa majukumu.
Bw. Bomphe alisema Ofisa Mtendaji Kata ya Kwediboma, Bw. Mohamed Kimweri, aliyekuwa amesimamishwa alirudishwa kazini.
CHANZO MAJIRA
0 comments:
Post a Comment