Home » » CCM yapoteza diwani

CCM yapoteza diwani

DIWANI wa Kiomoni, Masota Mayala (CCM), amefariki dunia juzi kutokana na maradhi ya mapafu na ubongo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, mtoto  wa marehemu, Kelvin Mayala, alisema kifo cha baba yake kimetokea ghafla na ni pigo kubwa kwao.
“ Kifo cha baba yetu ni pigo kubwa kwetu na familia kwa ujumla kwani alikuwa ni nguzo katika maisha yetu,” alisema Mayala.
Alisema baba yao alianza kusumbuliwa na maradhi hayo tangu mwezi uliopita na alikwenda katika Hospitali ya Masana, iliyopo Mbezi, Dar es Salaam kwa uchunguzi zaidi.
Katibu wa CCM wa Wilaya ya Tanga, Lusia Mwiru, alisema kifo hicho ni pigo kubwa kwao na serikali kwa ujumla, kwani diwani huyo alikuwa ni mwadilifu na mchapa kazi.
Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Halima Dendego alisema wilaya yake na CCM waimepata pigo kwa kumpoteza diwani huyo ambaye alikuwa mshauri mkubwa wakati wa kutekeleza ilani ya chama hicho.
Alisema mazishi ya Diwani Mayala yamefanyika jana katika kata hiyo.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa