Home » » WALEMAVU TANGA WAHITAJI VITAMBULISHO

WALEMAVU TANGA WAHITAJI VITAMBULISHO

JAMII ya watu wenye ulemavu mkoani Tanga wameiomba serikali kuwatengenezea vitambulisho maalumu vitakavyawawezesha kupata huduma za kijamii bila manyanyaso kutoka kwa baadhi ya watumishi wa umma wasiojali ulemavu wao.
Hatua hiyo ya walemavu hao kudai vitambulisho inatokana na miongoni mwao kudai kutotendewa haki kwenye huduma za matibabu hususani katika vituo vya afya na daladala ambako wamekuwa wakidharauliwa utu wao.
Kwenye kikao maalumu cha maandalizi ya rasimu inayohusu huduma za afya kwa watu wenye ulemavu wajumbe wa kikao hicho pamoja na mambo mengine wamejadili kwa kina kuhusu mustakabali wa maisha yao katika kupata huduma za kijamii bila kujali hali zao za ulemavu.
Lakini katika hali ya kustaajabisha na iliyowaacha midomo wazi wajumbe wa kikao hicho Mwenyekiti wa Chama cha walemavu mkoani Tanga Zuhura Musa na M/kiti wa chama hicho taifa Shida Salimu wametofautiana mtizamo na wajumbe hao kuwa vitambulisho vinazidisha unyanyapaa dhidi yao.            
Kwa upande mwingine Katibu wa Chama cha Albino nchini Ziada Sembu anawataka walemavu wote bila kujali aina za ulemvu wao kuungana ili kutetea haki haki zao kwa madai kuwa juhudi hizo zimeanza kuzaa matunda ya kuheshimika kwenye jamii na kushirikishwa kwenye vyombo vya maamuzi.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa