Home » » TBL YAKABIDHI VISIMA 15 KWANGWE

TBL YAKABIDHI VISIMA 15 KWANGWE

KAMPUNI ya Bia nchini TBL imekabidhi visima 15 vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 40 ilivyochimba katika vijiji vinne vya kata ya Kwamgwe wilaya ya Handeni mkoani Tanga ikiwa ni sehemu mojawapo ya kutumia sehemu ya faida yake kwa shughuli za kijamii.
Kukamilika kwa visima hivyo ni mojawapo ya ahadi ya kampuni hiyo iliyoitoa mwezi Octoba mwaka jana ambavyo vimechimbwa kwa usimamizi wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Tanga kwa msaada wa TBL.
Katika mahojiano na kituo hiki yaliyofanyika katika kijiji cha Bondo baadhi ya wakazi wa kata hiyo wameelezea furaha yao sanjari na kuishukuru TBL kwa kukubali kufadhili uchimbaji wa visima hivyo.
Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa TBL Bw. Steven Kilindo na msimamizi wa mradi huo Padre Edward Haule kutoka kanisa la Angilikana Dayosisi ya Tanga pamoja na mambo mengine wamewataka wakazi hao kuutunza badala ya kuhujumu miundombinu yake.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni Ramadhani Diriwa ameishukuru TBL kwa ufadhili wa mradi huo na kutoa rai kwa wananchi  kuutunza ili kampuni hiyo iweze kutoa ufadhili kwa maeneo mengine.
Takwimu zinaonyesha kuwa 56% ya wakazi wa wilaya ya Handeni hawapati huduma ya maji safi na salama licha ya jitihada mbalimbali zinazofanywa na wadau wa maendeleo ikiwemo TBL.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa