Home » » WATOTO WALIA NA ADHABU YA VIBOKO

WATOTO WALIA NA ADHABU YA VIBOKO



na Chalila Kibuda, Handeni
BARAZA la Watoto wa Kata ya Sindeni, wilayani Handeni, mkoani Tanga wameitaka serikali kuingilia kati adhabu ya viboko kutokana na walimu kupitiliza viwango na kuwafanya wanafunzi kusoma kwa woga.
Akizungumza na Tanzania Daima hivi karibuni, Mwenyekiti wa baraza hilo, Asnath Mbellwa, alisema adhabu ya viboko katika Kata ya Sindeni imekuwa tishio kwa wanafunzi na kusababisha kushuka kwa usikivu wakiwa darasani.
Alisema walimu wameipa adhabu hiyo majina ‘viboko vya supu’ na ‘dua’ na kusema kuwa haina lengo la kumfundisha mwanafunzi bali kumnyanyasa na kumdhalilisha.
“Viboko kwetu ndio kilio chetu kwa wanafunzi wa Sindeni na kuwafanya kusoma katika uwoga ambao mwisho wa siku mwanafunzi anakosa kujiamini,” alisema.
Naye Kaimu Ofisa Mtendaji, Amina Sikwatu, alisema atafuatilia kwa karibu juu ya viboko hivyo kwani serikali ilishapiga marufuku.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa