na Shehe Semtawa, Muheza
MKURUGENZI wa
Halmashauri ya Wilaya ya Muheza, Ibrahimu Matovu, amewatimua Ofisa Mtendaji wa
Kata ya Misalai, Mussa Chubwa na Mwenyekiti wa Chama cha NLD, Athuman
Abadallah, kwenye mkutano wa Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC), kutokana na
utovu wa nidhamu.
akizungumza na
Tanzania Daima mwishoni mwa wiki, mkurugenzi huyo alisema kutimuliwa kwa
watendaji hao kumetokana na kuonesha utovu wa nidhamu wakati Mkuu wa wilaya
hiyo, Subira Mgalu, alipokuwa akizungumza kwenye mkutano na watendaji wao,
kuhusu maendeleo ya wilaya hiyo.
Matovu alisema
wakati mkuu huyo wa wilaya (DC) akijadili agenda mbalimbali muhimu, alibaini
watendaji hao walikuwa wakibishana kuhusu kitabu cha mahudhurio ambacho ndiyo
ni maalumu kwa ajili ya posho za kikao.
Alisema
kutokana na watendaji hao kuendesha mkutano wao usio rasmi, hali hiyo ilimkera
na kuwatoa nje ya ukumbi.
Chanzo: Taaanzania Daima
0 comments:
Post a Comment