Mwandishi
wetu, Tanga Yetu
JESHI la polisi mkoani Tanga limetoa ufafanuzi kuhusiana na vitendo vya
mauaji vilivyotokea mwezi uliopita na kusababisha vifo vya watu 11 vilivyotokana
na sababu mbalimbali mkoani humo.
Hofu kubwa imetanda miongoni
mwa wakazi wa mkoa huo kutokana na vitendo hivyo ikiwemo kutekwa na kupotelea
katika mazingira ya kutatanisha hali ambayo imezua hofu na wengine kushindwa
kutembea nyakati za usiku.
Kamanda wa Polisi mkoani Tanga
Bw. Costantine Massawe amewaambia waandishi wa habari ofsini kwake kuwa vifo
hivyo vimetokana na sababu mbalimbali ikiwemo, wivu wa kimapenzi, wizi na
ulevi.
Amewataja waliopoteza maisha
katika kipindi cha siku kumi kuanzia Sept 14 hadi 24 kuwa ni Abdalah Athumani
(23) mwendesha bodaboda mkazi wa Tangasisi jijini Tanga, Mwajuma Kishi (31)
mkazi wa Chang’ombe Handeni, Rameck Jonas (35).
Wengine ni Kilo Husein mkazi wa
Chanika Handeni, Andrew Omar (82) mkazi wa Kwangema Mkinga, Shaban Zuberi (34)
mkazi wa Msambweni jijini Tanga, Ali Said (35-40) mkazi wa Kwafungo Muheza,
Frida Michael (22) mkazi wa Kwai Lushoto.
Wengine majina yao
hayakufahamika mara moja.
Blogzamikoa
0 comments:
Post a Comment