Home » » WANAFUNZI ECKERNFORDE TANGA WAANDAMANA

WANAFUNZI ECKERNFORDE TANGA WAANDAMANA

Mwandishi wetu, Tanga Yetu
ZAIDI ya wanafunzi 800 wa shule ya sekondari Eckernforde iliyopo jijini Tanga wameandamana hadi kwenye ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa jiji hilo wakidai kupatiwa ufumbuzi wa matatizo yao ikiwemo kutofundishwa kwa zaidi ya miezi mitano sasa.
Hatua hiyo inafuatia malalamiko ya wanafunzi waliyoyatoa kwa uongozi wa shule hiyo kushindwa kutatuliwa huku wengine wakirudishwa nyumbani kwa kushindwa kulipa ada na kukosa vipindi darasani.
Tanga Yetu imeshuhudia wanafunzi hao kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne wakirandaranda mitaani ambapo katika mahojiano wamesema wameamua kudai haki yao kwa maandamano baada ya utatuzi wa mezani kushindikana.
Hata hivyo msemaji wa taasisi ya Elimu Eckernforde Bw. Nyero Msagati amekiri kuwepo kwa malalamiko ya wanafunzi hao na kuahidi kupatiwa ufumbuzi haraka iwezekanavyo.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo Bw. Remency Tarimo amesema kuwa matatizo hayo yatapatiwa ufumbuzi lakini akawalaumu wanafunzi kwa uamuzi wa kufanya maandamano.
Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa