Home » » ZAIDI YA WAKAZI 3000 JIJINI TANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA MAJI YA TANGA UWASA

ZAIDI YA WAKAZI 3000 JIJINI TANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA MAJI YA TANGA UWASA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

ZAIDI ya wakazi 3000 wanaoishi katika eneo la Jaribu tena na Mwisho wa Shamba kata ya Maweni Jijini Tanga wanatarajiwa kuepukana na adha ya uhaba wa maji safi na salama iliyodumu kwa muda mrefu baada ya Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa mazingira Jijini Tanga kuwa pelekea mradi wa maji.
 
Akizungumza na waandishi wa habari Mkurungenzi Mtendaji wa Tanga UWASA Mhandisi Joshua Mgeyekwa alisema kuwa mradi huo unaotarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Septemba mwaka huu.
 
Alisema kuwa gharama za mradi huo hadi kukamilika kwake ni kiasi cha sh Mil98,lakini kutoka na gharama kuwa kubwa waliwashauri  wananchi ili kuona namna watakavyoweza kufanya kazi za kujitolea ili kukamilika kwa wakati.
 
Alisema kuwa ndipo wananchi walipoamua kushiriki katika kazi za kuchimba mitaro ambayo itaweza kutumika kwa ajili ya kupitisha miundombinu ya mabomba kutoka Pongwe hadi katika maeneo hayo yenye uhitaji.“tunawashukuru wananchi kwa ushirikiano waliounyesha wa kushiriki kwenye uchimbaji huo kwani wameweza kuokoa kiasi cha sh Mil 10 ambazoingebidi tuwalipe vibarua kwa ajili ya uchimbaji wa mitaro hiyo”alisema Mgeyekwa.
Alisema kuwa mradi huo umegawanyika katika awamu ambapo katika awamu ya kwanza unatarajiwa kusambaza maji katika umbali wa Km 5.5 kutoka eneo la Pongwe hadi katika mitaa ya Jaributena na Mwisho wa shamba.Nae Mbunge wa Jimbo la Tanga Mussa Mbaruku alisema kuwa kukamilika kwa mradi huo kwa haraka kutaweza kusaidia wananchi hao kuepukana na adha ya ukosefu wa maji iliyodumu kwa muda mrefu.
“Niwapongeze wananchi wa kata ya Maweni namna walivyoweza kujitolea kushirikina na serikali yao katika kumaliza changamoto zinazowakabili kwani hii inaonyesha kuwa ili kuharakisha maendeleo ya sehemu husika kunahitaji ushirikishwaji wa pande zote”alisema Mbunge Mbaruk.

Kwa upande wake Mtendaji wa Kata wa mtaa wa kichangani Ziada Ali alisema kuwa wakazi wa mtaa huo walilazimika kutembea umbali wa Km 5kwa ajili ya kutafuta huduma hiyo kila siku.
Alisema kuwa mradi huo utakapo kuwa umekamilika itakuwa ni faraja kwa wananchi wa mitaa ya Jaribu tena na Mwishi wa shamba pamoja na kuwapunguzu adha ya kwenda mwendo mrefu kwa ajili ya kutafuta huduma ya maji.

Vile vile Mwenyekiti wa Kamati ya Maji  Lucas Nyengo alisema kuwa kwa takribani miaka minne wamekuwa wakiomba kupatiwa huduma hiyo lakini wanashukuru kwa awamu hii kupatiwa mradi huo.
Alisema kuwa kufuatia shida ya maji ilidumu kwa muda mrefu waliamuakuunga mkono jitihada za mamlaka kwa kushiriki katika uchimbaji wa mtaro ili kuharakisha mradi huo.

Alisema kuwa kutokana na shida ya maji iliyokuwa inawakabili
walilazimika kununua  ndoo moja kwa kiasi cha sh 500 jambo ambalo ni gharama kubwa ukilinganisha na uhitaji wa huduma hiyo
Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa