Home » » Watendaji wa Mikoa, Wilaya na Halmashauri watakiwa kuanzisha Kamati za Michezo

Watendaji wa Mikoa, Wilaya na Halmashauri watakiwa kuanzisha Kamati za Michezo



Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura (kushoto) akisikiliza taarifa ya uwanja alipofanya ziara ya kutembelea uwanja  uliyowekewa jiwe la msingi na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) uliyopo eneo la Mtaa wa Makoko Ndumi ,Kata ya Mnyanjani kwa ajili ya kujenga uwanja wa michezo wa kimataifa  kwa kushirikiana na FIFA kutoka kwa Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Mhe.Mustapha Selemani leo Jijini Tanga alipotembelea alipofanya ziara ya kikazi kufuatilia maendeleo ya  shughuli za kisekta Mkoani hapo.

Anitha Jonas- MAELEZO
Tanga

Watendaji  wa Mikoa, Wilaya na Halmashauri watakiwa kuanzisha Kamati za Michezo  zitakazofanya kazi kwa ukaribu na Baraza La Michezo Taifa (BMT).
Agizo hilo limetolewa leo jijini Tanga na Naibu Waziri Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Annastazia Wambura  alipotembelea  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa  kwa ajili ya ziara ya kikazi yenye lengo lakutaka kujua maendeleo ya shughuli za kisekta kwa Wizara zinavyotekelezwa Mkoani hapo na changamoto zake.
“Kamati hizi za Michezo zitakapoundwa zitasidia kusimamia uendeshwaji wa Michezo katika Mkoa pamoja na usimamizi wa Vilabu vya Michezo halikadhalika usimamizi wa vyama vya Michezo kwa kuhakikisha vinakuwa na Katiba pamoja kuzingatia uendeshaji wa shughuli zake kwa kupitia Katiba hizo ambazo zitatakiwa kuzingatia muongozo”,alisema Naibu Waziri Mhe.Wambura.
Pamoja na hayo Naibu Waziri huyo aliwasisitiza kuwa Watendaji wa Mkoa kufanya mchakato wa kupata Maafisa Michezo waliyotoka katika vyuo vya Michezo vya Serikali kwa lengo la Maafisa hao kuwa Walimu wa Michezo katika ngazi zote  ambapo watasaidia  ukuibua wa vipaji vya wanamichezo kuanzia ngazi ya Kata mpaka Taifa,na kuongeza kipato kwani michezo ni ajira.
Kwa upande wa Mshahiki Meya  wa Jiji la Tanga Mhe. Mustapha Selemani alimuomba Mheshimiwa Waziri kusaidia kuharakisha ujenzi wa uwanja wa Kimataifa wa FIFA ambao tayari umeshawekwa jiwe la msingi na Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) ambapo ujenzi wa kiwanja hicho unatarajiwa kufanywa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).
Naye Msemaji wa Timu ya African Sports ambaye alikuwa Meya wa Jiji la Tanga Bw.Salim Kisauji alisema Timu za mpira wa miguu Tanga zimekuwa na changamoto ya ukosefu wa fedha za uendeshaji na hicho ndiyo chanzo cha kushuka kwa daraja kwa timu hizo  katika ligi za taifa.
Pamoja na hayo Naibu Waziri Wambura alitoa pongezi  Mwalimuwa Mpira wa Basketi Bw. Hemed Rajabu kwa jitihada walizozifanya zakuibua vipaji vya vijana na kuwasidia vijana 6 kupata nafasi za kusomeshwa Chuo Kikuu bure na wengine kupata nafasi ya kusomeshwa hata nje ya nchi bure ikiwemo nje  pamoja na hao waliyoko katika shule za sekondari.
Hata hivyo viongozi wa Timu za soka Mkoa wa Tanga wametakiwa kufanya jitihada za kupata mapato ikiwemo kuanzisha michezo ya bahati na sibu katika michezo yao kwa lengo la kupata fedha za kujiendesha.
           *************************MWISHO************************



0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa