Home » » URITHI WA TANGA

URITHI WA TANGA





Anitha Jonas – MAELEZO
Tanga    

Serikali imepongeza taasisi isiyo ya Kiserikali ya Makumbusho  Urithi  Tanga  kwa jitihada nzuri walizofanya za kuandaa makumbusho itakayo hifadhi utamaduni wa wakazi wa Mkoa wa Tanga.
Pongezi hizo zimetolewa leo jijini Tanga na Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo alipotembelea Makumbusho hayo ya Urithi Tanga alipokuwa katika ziara yake ya kikazi mkoani  hapo iliyolenga kujua uendeshwaji wa shughuli za kisekta.
“Kazi hii ya ukusanyaji wa taarifa mbalimbali za wakazi wa Tanga kuanzia ngazi ya Makabila yote saba ya Mkoa wa Tanga,Mila  na Desturi zao, pamoja na kuhimiza ukarabati majengo ya kale kweli mnahitaji pongezi kwa uzalendo huo”,
“Serikali ya China iliahidi kusaidia kujenga Majumba ya Makumbusho kwa nchi za Afrika hivyo andikeni barua ya Wizarani kuwa ajili ya kuendeleza makumbusho haya halafu tutaiwasilisha Ubalozi wa China”.alisema Naibu Waziri Wambura,
Kwa upande Mkurugenzi wa  Makumbusho ya Urithi  Tanga Mhandisi Godwin Mhando alisema lengo la kuanzisha makumbusho hayo ilikuwa ni kutaka kutunza historia ya Mkoa wa Tanga pamoja na kulinda kuhifadhi Mila na Desturi za watu wa Tanga kwa ajili ya vizazi vijavyo kwani Mkoa huo unahistoria  kubwa katika nchi.
“Makumbusho haya ya Urithi Tanga siyo kwa maslahi binafsi bali kwa wanatanga wote na tumeamua kufanya uhifadhi huu kwa  kuwa  tumeona ipo haja ya kuhifadhi historia Mkoa wetu.”alisema  Mhandisi Mhando.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa alisema  ofisi yake itajitahidi kushirikiana na viongozi wa makumbusho hayo kwa kuhakikisha inafikia malengo iliyojiwekea kwa maslahi ya wakazi wa Tanga pamoja na Watanzania wote kwa ujumla.
Aidha Mkurugenzi huyo wa makumbusho aliendelea kusema kupitia ofisi hiyo wamekuwa wakipanga siku ambayo hufanya maonesho ya shughuli za kiutamaduni kama matibabu ya kiasili,kuwepo kwa vyakula vya asili hii ikiwa ni siku ya maadhimisho  ya kuenzi utamaduni wa wakazi wa Tanga.
Hata hivyo kila Mtanzania  ametakiwa kujali asili yake pamoja utamaduni wake na pia kuenzi kwani ni urithi mkubwa kwa vizazi vijavyo.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa