Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Diwani wa Kata ya Usagara (CCM), Callos
Hizza katikati ya wiki hii alitoka nje wakati Mkutano wa Baraza la
Madiwani wa Jiji la Tanga ukiendelea kama ishara ya kupinga kupitishwa
mchoro wa Ramani ya Usagara Mashariki, akidai umelenga kupora eneo la
kata yake.
Mchoro huo uliwasilishwa katika mkutano wa baraza
hilo na Halmashauri ya Jiji la Tanga, ukitambuliwa kuwa ni wa Usagara
Extra namba 2/TA/382/G5.
Hata hivyo, diwani huyo alipinga na kudai wananchi
wa kata yake hawakubaliani na njama zinazofanywa kuwapora eneo lao Plot
615 block Z.
Awali, Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi na Mazingira,
Danny Mgaza alieleza kwamba mchoro huo umeandaliwa katika eneo la
Usagara ikiwa ni marekebisho ya mchoro wa Mipango Miji ya mwaka 1982 ili
kufanya uendane kiusahihi na hali halisi ya sasa.
Baada ya kusomwa ajenda hiyo, Diwani Hizza alisema
hakubaliani na akafafanua kuwa wataalamu wameupeleka katika mkutano huo
ili upitishwe kinyume na utaratibu, kwani ulishapimwa mwaka 2011 kwa
ajili maboresho ya eneo la Kata ya Usagara.
Licha ya kutoa ufafanuzi huo, baraza la madiwani
liliamua kuupitisha mchoro huo ndipo diwani huyo alipotoka nje kupinga
akidai kwamba angeendelea kukaa angekuwa ameshiriki kuwahujumu wananchi
wake.
“Wananchi wa Usagara tuna shaka na uhalisia wa
kuwasilisha mchoro huu. Tunashuku kwamba eneo lengwa halipo Kata ya
Mzingani bali lipo Usagara Kijijini, eneo mkabala na maghorofa ya
Bandari na waliomba kwa ajili ya ujenzi wa shule ya kata au viwanja vya
michezo,” alisema Hizza.
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment