Home » » Watakiwa kuhifadhi vifungashio

Watakiwa kuhifadhi vifungashio

Wananchi wametakiwa kuwa makini na vocha za pembejeo za kilimo wanazotumia kwa kuhifadhi vihifadhio vya mbolea hizo ili kudhibiti wauzaji bandia iwapo mbegu au mbolea walizotumia hazitakuwa na ubora.
Kaimu Ofisa Kilimo Halmashauri ya Wilaya ya Handeni, Yibarila Chiza alitoa tahadhari hiyo juzi alipokuwa akitoa maelekezo ya kugawa vocha za pembejeo za kilimo kwa wataalamu mbalimbali wa Tarafa ya Sindeni.
Chiza alisema kumekuwa na tabia ya baadhi ya kampuni kutoa mbolea za kupandia na mbengu za kukuzia, ambazo hazina ubora hivyo ni vyema wakulima kuhifadhi vya pembejeo hizo hadi mwisho wa msimu wa kilimo.
Alisema wamekuwa wakipata malalamiko kutoka kwa baadhi ya wakulima kuwa, mbolea au mbegu huwa hazina ubora hivyo kushindwa kupata mavuno ya kutosha kama walivyokusudia.
“Mnatakiwa kuwa makini na mbolea na mbegu bandia, mtunze vifungashio vya pembejeo hizo hadi mwisho wa msimu wa kilimo,” alisema Chiza na kuongeza:
“Kama pembejeo hizo zitakuwa na matatizo tuweze kuwawajibisha wahusika kwani wamekuwa wakiwapatia hasara kwa kutumia pembejeo zisizo na ubora.”
Pia, aliwataka watendaji wa vijiji, tarafa na kata kutokuwapa pembejeo hizo wakulima wenye uwezo kwani zimetolewa kwa ajili wa wakulima wenye kipato cha chini.
Alisema pembejeo hizo ni kwa wale ambao hawajiwezi, lengo likiwa ni kuwasaidia kulima kilimo chenye tija.
Chanzo;Mwananchi
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa