Home » » RC aitaka halmashauri kushikiriana

RC aitaka halmashauri kushikiriana

 Halmashauri ya jijini hapa imetakiwa kushirikisha wananchi pamoja na sekta binafsi katika miradi ya maendeleo ili kuleta matokeo bora na ya haraka pamoja na kuchochea kasi ya mabadiliko ya kiuchumi.
Ushauri huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa wakati wa ziara yake katika Kata ya Kati(Central) iliyokuwa na lengo la kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwenye kata hiyo.
Alisema, halmashauri hiyo bila ya kushirikisha wadau hasa wa sekta binafsi haitaweza peke yake  kutoa huduma sambamba na kuleta maendeleo na mabadiliko kwenye shughuli mbalimbali hasa za kijamii.
“Halmashauri ya Jiji la Tanga tuache umangimeza kwa kutaka kila kitu tufanye wenyewe, ni lazima ifike mahali mtoe nafasi kwa sekta binafsi kuwasaidi katika shughuli za kimamendeleo na nyie mbakie kwenye ukaguzi pekee,”alisema Gallawa.
Aliongeza kuwa halmashauri ndiyo yenye wajibu wa kuandaa mazingira ya ajira katika ngazi zote kuanzia kwenye mitaa hadi Jiji na kuwashauri waandae mazingira ya ajira kwa vijana badala ya kung’ang’ania kila jambo.
Akizungumzia suala la usafi wa jiji , Gallawa aliwashauri kuwaachia vijana kazi hiyo ili waweze kujiajiri na halmashauri wabaki na jukumu la kusimamia pamoja na kukagua.
Awali Ofisa Usafishaji wa Jiji, Sylvester Magobo akitoa taarifa ya hali ya usafi, alisema jiji linakadiriwa kuzalisha wastani wa tani 240 za taka ngumu kila siku na kuhifadhiwa kwenye maeneo ya uzalishaji kwa hivi sasa.
Alisema wanakabiliwa na changamoto za upungufu wa vifaa vya mifumo ya uendeshaji ambapo uboreshaji wake utawezesha maeneo yote kupata huduma yenye mitiririko imara na wa haraka.
“Uwezo wa jiji ni kukusanya taka kwa kiwango cha asilimia 84 ya taka zinazozalishwa katika kata 14 za mjini hapa,hivyo bado tunakabiliwa na upungufu wa vifaa vya kuzolea vilivyo na ubora,”alisema na kuahidi kujipanga vyema.
Chanzo;Mwananchi
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa