Home » » Wazee Muheza waomba uzio

Wazee Muheza waomba uzio

WAZEE wanaoishi kwenye kambi ya ukoma iliyopo Ngomeni, wilayani hapa, wameiomba serikali kuwajengea uzio ili kuwanusuru na vibaka wanaowavamia mara kwa mara na kupora mali zao, ikiwemo mifugo.
Walitoa ombi hilo wakati  wakipokea msaada wa nguo na chakula kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Tanga  wakati ilipotembelea kambi hiyo.
Walisema kambi hiyo ipo mbali na makazi ya watu, hivyo inakuwa rahisi kwa vibaka na wezi kuwavamia mara kwa mara, hasa katika kipindi wanachopelekewa misaada.
“Tunaiomba serikali ituangalie katika suala la kujengewa uzio na uhakika wa majisafi na salama, kwani kwa sasa hakuna, inatulazimu kwenda mwendo mrefu kutafuta maji. Bwawa lililochimbwa kwa ajili yetu limekauka,” alisema  Mohamed Salimu.
Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Mathew Mganga, alisema kambi hiyo ina wazee 86 ambao wanatumia matundu matatu ya vyoo ambayo hayalingani na idadi yao.
Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Tanga, Edson Makallo, alisema iwapo watendaji kwenye ngazi zote wangeweza kusimamia fedha za maendeleo na kuhakikisha zinawafikia walengwa, rushwa nchini ingepungua au kwisha kabisa
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa