Home » » TRA waaswa kutoa huduma bora

TRA waaswa kutoa huduma bora



MAMLAKA  ya Mapato  (TRA) imetakiwa kutoa huduma bora ili kuwafanya walipa kodi walipe kwa hiari, hivyo kuongeza pato la serikali na kukuza uchumi wa taifa.
 Imeelezwa kuwa elimu wanayotoa kwa walipa kodi ni muhimu, hivyo inatakiwa kutolewa mara kwa mara na kuongeza kuwa uelewa wa mlipa kodi juu ya sheria na taratibu za  kodi wanazolipa utawafanya walipe kodi zao kwa hiari.
 Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Halima Dendego alipokuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa maadhimisho ya saba ya Siku ya Mlipa Kodi yaliyofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Bombo, mjini hapa.
 Dendego alisema  mamlaka hiyo inatakiwa kutoa huduma bora kwa walipa kodi na wananchi wa Tanzania kwa lengo la kukusanya mapato ya serikali kwa kiwango kikubwa.
Kwa upande wake, Meneja wa TRA mkoani hapa, Nyonge Mahanyu, alisema wanatumia siku hiyo kuwakumbusha wafanyabiashara kulipa kodi kwa hiari, kwa wakati na kutoa risiti.
Awali katika uzinduzi huo mkoani Tanga imetoa msaada wa shuka 100 katika   Hospitali ya Bombo, zenye thamani ya sh milioni 1.6.
 Akizungumza baada ya kupokea msaada huo, Mganga Mfawidhi wa hospitali  hiyo,  Dk. Jumanne Karia,  alitoa wito kwa wanaotaka kutoa misaada wawashirikishe ili waweze kueleza hitaji lao, kwani hospitali ya mkoa huo ina ukosefu wa vifaa vingi.

Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa