Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC)
Agizo hilo limetolewa na Mwenyekiti wake, Rajabu Mbarok kwenye ziara ya wajumbe wa kamati hiyo iliyofanyika wilayani hapa ambayo iliambatana na ukaguzi wa miradi ya maendeleo.
Alisema Mwanasheria huyo ambaye kwa sasa amehamishiwa katika halmashauri nyingine ya wilaya iliyopo mkoani humo anastahili kupewa onyo kali kwa kitendo chake cha kuifanya halmashauri ya Muheza kushindwa katika kesi hiyo dhidi ya wafanyakazi wake.
Alisema kitendo cha mwanasheria huyo kushindwa kuitetea halmashauri hiyo mahakamani kimewapa ushindi wafanyakazi hao na kurudishwa kazini.
Awali akitoa taarifa mbele ya kamati hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu alisema kwa halmashauri ya wilaya hiyo imepata hati safi kwa miaka mitano mfululizo katika hesabu za serikali.
Alisema halmashauri hiyo imekuwa ikipata hati safi za mahesabu kila wakikaguliwa na mkaguzi wa mahesabu wa nje.
Alisema kutokana na uaminifu wa kutumia fedha za serikali vizuri katika miradi, wataendelea kupata hati safi kila mwaka.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mbarok alipongeza jitihada zao hizo na kuwataka kutumia fedha zinazoletwa na serikali kwa miradi iliyokusudiwa ili wananchi wapate maendeleo.
Naye Mwakilishi wa Ukaguzi wa Mahesabu ya Serikali (CAG) wa Nje aliyejitambulisha kwa jina moja la Christopha, alisema kuwa wamepokea taarifa za mahesabu kutoka halmashauri hiyo lakini bado taarifa nyingine hazijakamilika.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment