Home »
» Chanzo cha umaskini chabainishwa
Chanzo cha umaskini chabainishwa
|
|
IMEELEZWA kuwa chanzo cha umaskini nchini ni mahusiano mabaya kati ya viongozi wa kuchaguliwa na wananchi wa maeneo husika.
Wakiuzungumzia kwa nyakati tofauti wakati wa mahojiano na gazeti
hili baadhi ya wananchi ambao ni wakazi wa vijiji mbalimbali
wilayani hapa, walieleza kuwa viongozi ndio tatizo na chimbuko la
kudumu kwa maendeleo nchini.
Mmoja wa wananchi hao, Sadick Ramadhan, alisema viongozi wanaodumaza
maendeleo ni wale walioingia madarakani kwa mizengwe wakiwa na lengo
la kujinufaisha badala ya kuwanufaisha wananchi waliompa ridhaa ya
kuwaongoza.
Naye Nassoro Mojera alisema rushwa katika uchaguzi, ndiyo tatizo la
viongozi wanaotangazwa na tume ambao si chaguo la wananchi.
Mojera aliongeza kuwa kutokana na viongozi kupatikana kwa njia ya
rushwa na kutokuwa na ridhaa ya wananchi ni vigumu kujenga mahusiano
ambayo yangewawezesha kukaa pamoja na kujadili maendeleo yao.
Yassin Kabelwa yeye alieleza sababu mbalimbali zinazochangia
kuvunjika kwa mahusiano baina ya viongozi na wananchi na kuzitaja
baadhi kuwa ni ubinafsi wa viongozi, na ushabiki wakati wa uchaguzi.
CHANZO;TANZANIA DAIMA
|
|
0 comments:
Post a Comment