Home » » RC awapa changamoto wakazi Tanga

RC awapa changamoto wakazi Tanga

MKUU wa Mkoa (RC) wa Tanga, Luteni mstaafu Chiku Gallawa, amewataka wakazi wa Jiji la Tanga na maeneo ya jirani kuchangamkia ajira zinazotolewa na Kiwanda cha Saruji cha Rhino kilichopo katika Kata ya Maweni jijini hapa.
Gallawa alitoa ushauri huo baada ya kutembelea eneo la kiwanda hicho na kushuhudia ujenzi unaoendelea, ambapo alielezwa kuwa itakapofika Julai mwakani kiwanda hicho kitakuwa kimeanza uzalishaji.
Mkuu huyo wa mkoa alielezea lengo la kufanya ziara yake kiwandani hapo ni kutaka kujua changamoto zinazokikabili kiwanda hicho alichoeleza kuwa kitakapokamilika kitakuwa kimepunguza tatizo la ajira kwa wananachi.
“Ndugu zangu sisi kama mkoa tunataka mmalize haraka ujenzi wa kiwanda hiki ambacho kitakuwa chachu ya maendeleo ya ajira mkoani hapa na taifa kwa ujumla,” alisema Gallawa.
Kwa upande wake mmoja wa wamiliki wa kiwanda hicho, Sudheer Khaqram, alisema kiwanda hicho kitakapokamilika watakuwa wamekwisha kuajiri watu wa jinsia zote kutokana na mchakato wa kutoa ajira unaoendelea kiwandani hapo kwa sasa.
“Tunatarajia kuwa na wafanyakazi 300, kwa sasa waliopo ni 100, ni fursa nyingine ya ajira kwa wakazi wa Tanga na maeneo ya jirani,” alisema Khaqram.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa