Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akihutubia katika sherehe za Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wazee
Duniani, zilizofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Mazoezi Wilaya
ya Korogwe Mkoani Tanga jana.
Makamu
wa Rais, Dkt. Bilal, akivishwa vazi la asili la kabila la Wadigo, na
Mwenyekiti wa Umoja wa Wazee wa Wilaya ya Korogwe, Abdallah Semkiwa,
wakati wa sherehe za kilele cha Siku ya Wazee Duniani, zilizofanyika
mkoani Tanga.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akiagana na baadhi ya Wazee waliohudhuria katika sherehe za Kilele cha
Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani, baada ya kuhutubia katika sherehe
hizo zilizofanyika kwenye Uwanja wa Mandu, Korogwe Mkoani Tanga jana
Okt. 01, 2013. (Picha na OMR).
0 comments:
Post a Comment