Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Na Dotto
Mwaibale, Tanga
WAZIRI Mkuu
Mizengo Pinda leo anatarajia kufungua mkutano wa kimataifa wa uwekezaji Kanda
ya Kaskazini utakaofanyika mkoani hapa.
Akizungumza
katika mkutano na waandishi wa habari leo Mkuu wa Mkoa huo Luteni mstaafu
Chiku Gallawa alisema mkutano huo wa siku mbili utakaofanyika leo na kesho utatoa
fursa ya kukuza uchumi wa mkoa wa Tanga.
“Mkutano huu
utahudhuriwa na wawakilishi wa nchi zote zenye balozi hapa nchini na utafanyika
Hoteli ya Mkonge mjini hapa” alisema Gallawa.
Alitaja
mikoa iliyopo katika kanda hiyo itayoshiriki mkutano huo kuwa ni Arusha,
Manyara, Kilimanjaro na Tanga ambao ni mwenyeji.
Alisema
mkutano huo utatoa nafasi ya wananchi kuzitambua fursa zilizopo ambazo
hazijafahamika vizuri kupitia wawekezaji hao.
Alisema
maandalizi yote ya kuzitambua fursa zilizopo mkoani humo tayari yamefanyika na
zitawekwa wazi katika mkutano huo ili kila mwananchi azielewe.
Alisema kuna
fursa nyingi ambazo zinahitajika uwekezaji kwa ajili ya kuinua uchumi wa mkoa
wa Tanga na nchi ambapo alizitaja kuwa ni sekta ya kilimo, madini, ufugaji
ambako kuna maeneo mengi ya malisho kama wilayani Handeni kwenye mashamba ya
malisho 10 na Korogwe ambako kuna madini ya Jimsam yanayotumika kutengenezea
chaki, unga wa kufungia mtu aliyevunjika ‘POP’ , chokaa na saruji ambayo yapo
Kata ya Mkomazi.
“Wenzetu
kutoka nje wana utalaamu na fedha na sisi tuna ardhi, rasilimali, miundombinu
mizuri kama umeme na barabara hivyo ni vema kuchangamikia fursa hizo” alisema
Gallawa.
Alisema
katika mkutano huo kutakuwa na maonesho ya bidhaa mbalimbali zinazozarishwa na
viwanda vilivyopo Tanga na zile za asili zinazotengenezwa na wenyeji wa mkoa
huo.
Gallawa amewaomba
wananchi wa mkoa wa Tanga kupitia vyombo vya habari kujitokeza kwa wingi
kushiriki katika mkutano na kumpokea Waziri Mkuu Mizengo Pinda atakayekuwa
mgeni rasmi.
Alisema
maandalizi yote kuhusu mkutano huo yamekamilika kwa kushirikiana na Halmsahauri
zote za wilaya za mkoa huo.
0 comments:
Post a Comment