Home » » Trafiki Tanga waonywa kupokea rushwa

Trafiki Tanga waonywa kupokea rushwa

MKUU wa Mkoa wa Tanga, Luteni Mstaafu Chiku Gallawa amewaonya askari wa kitengo cha usalama barabarani kuacha tabia ya kupokea rushwa kutokana na makosa yanayofanywa na madereva kwani kufanya hivyo ni kulidhalilisha Jeshi la Polisi.
Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa Wiki ya Nenda kwa Usalama, iliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Tangamano, jijini Tanga na kitaifa mkoani Mwanza.
Gallawa alisema baadhi ya trafiki ambao sio waaminifu, wamekuwa wakiwaomba rushwa wanapokuwa barabarani na matokeo yake wanadhalilisha jeshi kwa kulipaka matope hivyo ni vema kuacha tabia hiyo.
Hata hivyo, ameitaka Halmashauri ya Jiji la Tanga kukarabati miundombinu ya barabara ili kupunguza ajali zisizo za lazima kwa wananchi.
Mbali na hayo, pia amewataka wananchi kuwafichua watu wanaoiba miundombinu ya barabara kwa kuifanya vyuma chakavu matokeo yake ajali zinazidi kuongezeka.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa