Home » » GANGSTAR RECORDS KUREKODI BURE NYIMBO ZA WASANII CHIPUKIZI TANGA

GANGSTAR RECORDS KUREKODI BURE NYIMBO ZA WASANII CHIPUKIZI TANGA

Majanga ya ukata yanayowakumba wasanii wengi wanaochipukia katika muziki wa kizazi kipya na hivyo kushindwa kuingia studio kurekodi nyimbo zao yamepata mkombozi baada ya studio ya Gangstar records ya jijini Tanga kutangaza kurekodi nyimbo za wasanii hao bure.
 Producer Dan (kushoto) akiwa na mwandishi wa habari Dotto Kahindi

Producer wa studio hiyo Dan amesema wameamua kufanya hivyo ili kutoa fursa kwa wasanii wenye vipaji kurekodi nyimbo zao na hivyo kuonyesha vipaji vyao kwa jamii.

Mkoa wa Tanga ni miongoni mwa mikoa michache yenye wasanii wenye vipaji imefanikiwa kutoa wanamuziki kama akina Matonya, Suma Lee, C pwaa, Mkoloni, TNG, Roma mkatoliki, na wengine kibao.

Hawa ni wale ambao wamefanikiwa kutoka na kutambulika katika maeneo mengine nje ya mkoa huo, lakini kuna msululu mrefu wa wasanii tena wenye vipaji ambao hawajapata nafasi ya kuonyesha vipaji vyao kutokana na kukosa sapoti ya kuingia studio lakini sasa wameipata nafasi hiyo.

 Cosh Cash

Tutegemee kupata vipaji vipya kutoka Tanga 2013

 
 Robby Kiss

Babylon

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa